• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maadhimisho ya Juma la Elimu Mkoa wa Tanga yafanyika kwa Vitendo

Imerushwa: April 28th, 2019


Maadhimisho ya juma la elimu Mkoa wa Tanga yamefanyika katika Wilaya Handeni tarehe 26-27/04/2019 ambapo siku ya kwanza wadau wa elimu kutoka Wilaya zote za MKoa walitembelea miradi ya elimu ya Wilaya ya Handeni ikiwepo ujenzi wa madarasa, mabweni, Maabara ya sayansi na shamba la shule lenye ekari zaidi ya 20 na baadaye walitembelea mabanda ya maonyesho ya taaluma na kugawa wa zawadi kwa shule zilizofanya vizuri kitaaluma kwa mwaka 2018. Siku ya pili kilifanyika kikao cha tathmini ya maendeleo ya elimu ya Mkoa katika ukumbi wa Makuti uliopo Wilayani hapo.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa miradi ya maendeleo ya elimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga ambaye pia alikuwa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo Mh. Martin Shigela aliwapongeza viongozi wa Wilaya ya Handeni na wananchi kwa jitihada wanazofanya kuhakikisha maendeleo ya elimu yanasonga mbele na kuahidi kuunga mkono juhudi hizo lakini pia alichangia mifuko ya simenti zaidi ya 300 na matanki ya kuvuna maji.

Wakati huo huo Mh. Shigela aliwaagiza Meneja wa TANESCO na TARURA kutengeneza miundo mbinu ya barabara na umeme katika shule za sekondari Kisaza ambayo inatarajiwa kuanzishwa kidato tano na sita na shule ya sekondari Kitumbi ambayo ni mpya iliyojengwa na wadau wa elimu ili kuwa na mazingira rafiki kwa wanafunzi kusoma hasa shule ya sekondari Kisaza ambayo ni ya bweni.

Mh. Shigela alipotembela shamba la shule ya Sekondari ya Komnyang’anyo lenye ekari zaidi ya 20 iliyopandwa mihogo, mahindi na korosho aliagiza kila Halmashauri kuiga mfano huo ili kuondokana na uhaba wa chakula shuleni kwani upatikanaji wa chakula una uhusiano mkubwa katika ufaulu wa wanafunzi.

Katika kikao cha tatmini ya maendeleo ya elimu ya Mkoa Mh.Shigela alitaka kila ngazi ya uongozi katika kila Halmashauri kufanya tatmini ya elimu kila mara ili kujua changamoto za maendeleo ya elimu mapema na kuzitatua kwa wakati ikiwepo suala la upatikanaji na chakula shuleni, utoro wa wanafunzi, suala la mimba kwa wanafunzi na maendeleo ya taaluma na michezo.

Aidha, Mh. Shigela aliwasihi viongozi wa ngazi ya Halmashauri, Kata na Vijiji kuwa na utamaduni wa kutoa motisha kwa walimu pale wanapoajiriwa katika maeneo yao ili waweze kupenda mazingira ya kazi na kupunguza tatizo la walimu kuhama. Alitoa agizo kwa kila Halmashauri kusimamia suala makambi kwa madarasa ya mitihani ili kuinua kiwango cha ufaulu.

Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Said amesema Halmashauri ziwe makini katika utoaji wa takwimu kwani wamekuwa wakikana takwimu kuwa siyo zao hivyo tatmini ya kina ifanyike, wajiridhishe na kusainiwa na Mkurugenzi ndipo ipelekwe ngazi ya mkoa.

Mhandisi Zena alipongeza Halmashauri kuboresha utoaji wa zawadi kwa shule zilizofanya vizuri na kuwasihi kuendelea kutoa hiyo hamasa lakini pia alipongeza suala la wadau wa elimu kuongegezeka katika tatmini ya elimu mwaka huu.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe alieleza jinsi ambavyo upatikananji wa chakula shuleni ulivyochangia ufaulu wa wanafunzi ambapo alisema mwaka 2016 ufaulu wa darasa la saba kwa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni ulikuwa asilimia 62 lakini walivyoanza kuhimiza utoaji wa chakula shuleni mwaka 2017 ufaulu ukaongezeka na kufikia 73% na mwaka 2018 ukafika 81.6% lakini pia alisema utoro wa rejareja wa wanafunzi ulipungua kwa kiwango kikubwa.

MWISHO.

Pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh.Martin Shigela akishindilia udongo alipotembela na kuona

 ujenzi wa bweni la shule ya Sekondari Kisaza Wilayani Handeni.

Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Said 

akizungumza katika kikao cha tathmini ya elimu Mkoa wa Tanga.

Mkuu wa Wilaya Handeni Mh.Godwin Gondwe wa tatu kushoto akifafanua jambo kwa Mkuu wa Mkoa.

Wadau wa Elimu wakifuatilia  tathmini ya elimu ya Mkoa wa Tanga.


Wadau wa Elimu wakisikiliza jambo kutoka kwa msimamizi wa mradi wa ujenzi Shule ya Sekondari Kisaza

 Bw. Mbazi Mfinanga wa kwanza kushoto.

Mwanafunzi aliyefanya vizuri kitaifa kutoka shule ya Tanga ufundi katika mahindano ya ubunifu akipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi.

Pichani ni Wanafunzi,Shule na Kata zilizofanya vizuri mitihani ya mwaka 2018 zikikabidhiwa zawadi.








Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa