• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mashindano ya usafi wa mazingira shuleni yafikia kilele

Imerushwa: August 6th, 2019


Kampeni ya usafi wa mazingira (National Sanitation Campaign) katika halmashauri ya wilaya ya Handeni ambayo ilishindanisha shule za Msingi na Sekondari imefikia kilele.

Katika kufikia kilele cha mashindano hayo kilichofanyika jana katika shule ya sekondari Kwalugulu washindi watatu wa shule za msingi na sekondari walipewa zawadi ya fedha na washindi wa jumla walipewa vyeti.

Akizungumza katika kilele hicho mgeni rasmi Bw. Francis Mashalo alisema kuwa suala la usafi ni suala la kitaifa na lilianza tangu mwaka 1973 kwenye Azimio la Arusha. Halmashauri ya wilaya ya Handeni ilianza kampeni hiyo tangu mwaka 2012 na matokeo chanya yalionekana.

Pia aliwataka wananchi wadumishe usafi katika maeneo yao ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko na alisisitiza wananchi kujenga vyoo bora vinavyotumika na kuzingatia usafi wa vyoo hivyo bila kusahau kunawa mikono baada ya kutoka chooni pamoja na kuchemsha maji ya kunywa.

Naye Afisa Elimu Sayansikimu ambaye ndiye mratibu wa kampeni hiyo Bi. Grace Mbanga alitaja maeneo muhimu yaliyozingatiwa ili kupata washindi ambayo ni uwepo wa vyanzo vya maji safi na salama, usafi wa mazingira ya shule, utupaji salama wa taka, uelewa wa watu juu ya magonjwa ya mlipuko na dengu, uelewa wa suala la hedhi salama, ubunifu, kutambua njia na mbinu za kujikinga na magonjwa.

Aliongeza kuwa katika kampeni ya usafi wa mazingira kitaifa ya mwaka 2012 wizara nne zilishiriki katika kampeni hiyo ambazo ni wizara ya afya kama mdau wa afya ya jamii, wizara ya maji kama mdau wa miundombinu bora ya maji safi na salama, wizara ya elimu kama jamii lengwa na wizara ya TAMISEMI kama mtunga sera.

Naye mwalimu wa baiolojia wa shule ya sekondari Kwalugulu madam Winifrida Akhoguti alisema wamefurahia mafundisho yaliyotolewa na wataalamu pamoja na zawadi zilizotolewa ambapo italeta chachu na ari ya usafi wa mazingira pamoja na kutoa elimu kwa jamii kuhusu suala la usafi wa mazingira.

Kwa upande wa mwanafunzi Said Mussa Msingwa aliahidi kutoa elimu hiyo ya usafi wa mazingira katika maeneo yao wanayoishi kwa wale ambao hawajapata elimu hiyo kwa kuwa uchafu wa mazingira unasababisha magonjwa ya mlipuko ambayo yanawaathiri watanzania wengi.

Washindi wa jumla ni pamoja na shule ya sekondari Kwankonje ambayo imeshika nafasi ya kwanza, shule ya msingi Nyasa ambayo imeshika nafasi ya pili na shule ya sekondari Kwalugulu ambayo imeshika nafasi ya tatu.

Mgeni rasmi Bw. Francis Mashallo akizungumza

Mratibu wa kampeni ya usafi wa mazingira Bi.Grace Mbanga akizungumza

Afisa Maendeleo ya jamii Bi.Thea Mauki akitoa elimu

Kitalu cha miti ambayo ni sehemu ya utunzaji wa mazingira shule ya Sekondari Kwalugulu

Mgeni rasmi Bw. Francis Mashallo akitoa zawadi kwa washindi.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kwaluguru wakisikiliza mafunzo 



Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa