Mkuu wa Mkoa wa Tanga MH. Martine Shigella Jana ametembelea chuo cha Jeshi la zimamoto kilichopo Kijiji cha Chogo Kata ya Kabuku Wilayani Handeni na kuwataka kudumisha ushirikiano baina ya jeshi na wananchi katika kuimarisha ulinzi na usalama.
Mkuu wa Mkoa ametembelea miundombinu ya Jeshi hilo la zimamoto ambapo kwa sasa Hakuna mafunzo yanayoendelea, maeneo aliyotembeleea ni Bwalo la Jeshi, kituo cha polisi, zahanati ya chogo na jiko la kupikia chakula.
Katika Ziara hiyo Mkuu wa Mkoa alipokelewa na mwenyeji wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni MH Godwin Gondwe , wataalamu mbalimbali na Kamati ya ulinzi na usalama.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigella Kipata maelezo mafupi kutoka kwa Bakari Mrisho mkuu wa chuo cha Jeshi la zimamoto
Mkuu wa Mkoa wa Tanga akifuatiwa na mkuu wa Wilaya ya Handeni wakitoka kuangalia bwalo la chuo hicho.
Mkuu wa mkoa na viongozi mbalimbali apikata melezo mafupi kwenye eneo la kupikia chakula.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe akifuatiwa na mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigella wakipata taarifa ya zahanati ya chogo.
Mkuu wa mkoa na viongozi wakiwa kwenye ziara.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa