• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Baraza la madiwani handeni yapata Mwenyekiti mpya

Imerushwa: February 5th, 2019

BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI YAPATA MWENYEKITI MPYA.

Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga imefanya mabaraza ya siku mbili, baraza la kawaida la robo ya pili ya mwaka na baraza maalumu ya kupitisha rasimu ya bajeti ya mwaka 2019/2020. Katika baraza la kawaida waheshimiwa madiwani walimchagua mwenyekiti mpya wa Halmashauri baada ya nafasi hiyo kuachwa wazi kwa muda wa  takribani miezi mitatu kufuatia mwenyekiti wa awali Mh.Diliwa kujiuzuru kutokana na kukataa kusaini muhtasari uliyokuwa unakipengele kinachosema maamuzi ya baraza ya kipindi hicho yaliyofanyika kuhusu makao makuu ya Halmashauri kujengwa Kabuku hayakuwa sahihi.

Uchaguzi huo ulifanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni ambapo diwani wa Kata ya Kwamatuku Mh. Mustafa Beleko  wa tiketi ya Chama cha Mapinduzi  alishinda kwa kura zote 22 ya idadi ya waheshimiwa madiwani waliohudhuria baraza hilo.

Aidha mwenyekiti huyo alipatikana baada ya katibu wa baraza hilo Bw. William Makufwe kuandika barua kwa vyama viwili  vya siasa ikiwepo Chama cha Mapinduzi (CCM) na CHADEMA na kupata majibu ya jina moja kutoka CCM. “Tuliandika barua kwa vyama viwili CCM na CHADEMA lakini mpaka leo tumepata barua moja kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) ambayo imeleta jina la mgombea moja kupitia Chama cha Mapinduzi”. Alisema Makufwe.

Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Mustafa Beleko aliwashukuru viongozi wa Chama cha Mapinduzi Wilaya na Waheshimiwa madiwani kwa kumwamini na kumweka katika nafasi hiyo na kuwaahidi kutowaangusha kwani amepata uzoefu wa kutosha kutoka kwa Mwenyekiti aliyepita.

Katika baraza maalumu la kujadili rasimu ya bajeti ya tarehe 05/02/2019 Baraza hilo lilipitisha kwa pamoja rasimu hiyo ya bajeti ya mwaka 2019/2020 kiasi cha shilingi bilioni 36.5.

Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bi. Edina Katalaiya akitoa mchanganuo wa bajeti hiyo alisema rasimu hiyo ya bajeti imefuata kanuni, taratibu na mwongozo wa kuandaa bajeti ya mwaka 2019/2020 kutoka Wizara ya fedha na mipango iliyotolewa mwezi Disemba 2018 na vikao vyote vya maamuzi vya Halmashauri.

Aliongeza kuwa rasimu hiyo pia imefuata mwongozo wa undaaji wa bajeti ya mishahara, ilani ya uchaguzi ya chama tawala (Chama cha Mapinduzi), mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano, mpango mkakati wa Wilaya na mpango wa uwiano wa mkoa. alisema kuwa bajeti hiyo ya billion 36.5 ni kwaajili ya miradi ya maendeleo, kulipia mishahara na matumizi mengineyo.









Waheshimiwa madiwani wakipiga kura ya kumchagua mwenyekiti katika baraza hilo.


Kura zikihesabiwa na mh.Muya wa kwanza kulia, Afisa Utumishi Bi. Kalovya(katikati)

na mwanasheria Bw.Mangesho(wa kwanza kushoto).


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ambaye pia ni katibu wa baraza 

Bw.William Makufwe akimvalisha joho  mwenyekiti Mh.Mustafa Beleko baada ya uchaguzi

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Mustafa Beleko akitoa neno la shukrani 

baada ya kushinda kwa kura zote za ndiyo.


Kaimu Afisa Mipango, Takwimu na ufuatiliaji Bi. Edina Katalaiya akisoma rasimu ya bajeti ya

mwaka wa fedha 2019/2020.





Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa