• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

Imerushwa: August 6th, 2024

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Handeni likiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Mussa Mwanyumbu limefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kwa lengo la kujifunza na kuongeza uwezo wa kuisimamia Halmashauri katika maswala ya Kiutawala , Uzalishaji wa Hewa ya ukaa, kubuni vyanzo vipya vya mapato.  kujifunza namna ya kuiendasha na sasa wanaenda kuhakikisha Halmashauri inakuwa kinara katika nyanja zote za ukuaji kiuchumi.


Baada ya kutembelea na kuona Miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Tanganyika Mhe. Mwanyumbu amesema kutokana Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kuwa kinara katika ukusanyaji wa mapato, mapato yatokanayo na mauzo ya Hewa ukaa hivyo chaguo lao limegusa mahitaji na wanenda kuyatumia yote waliyoyapata na kuboresha Ustawi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.


Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Albert Msando ambaye pia alikuwa ni Miongoni mwa waliofanya ziara hiyo amewataka Madiwani na Wataalam kutumia elimu ya  mafunzo waliyoipata ili iweze  kuboresha  ukusanyaji wa mapato kwa lengo la kuongeza  kiwango cha ukusanyaji wa mapato  katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.


Katika ziara hiyo Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini Mhe. John Sallu aliyekuwa miongoni mwa ziara hiyo amesema ziara hiyo imelenga kuwapatia mafunzo Madiwani kwa lengo la kuona wenzao namna wanavyozisimamia Halmashauri pamoja na namna ya kukusanya mapato.


Akizungumza wakati wa mapokezi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Alex Mrema ambaye ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika amesema kuwa tumeguswa na ziara yenu kwasababu  ziara hiyo itasaidia kuboresha utendaji wa kazi baina ya Halmashauri yatu pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni “ Aliwakaribisha”


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Saitoti Stephen amesema kwamba tumefanikiwa kufanya ziara katika Halmashauri ya Tanganyika na kujifunza namna  wanavyokusanya mapato yatokanayo na mauzo ya hewa ukaa, kuona mbinu za ukusanyaji Mapato ya Halmashauri, kuona jinsi vijiji vinavyonufaika na Mapato ya hewa ukaa ikiwa ni pamoja na wananchi zaidi ya 34,000 wamilipiwa bima ya afya katika vijiji 8.

.

Aidha Bw. Saitoti alisema ili kufanikisha  ukusanyaji wa mapato hayo inahitaji ushirikishwaji, kuwawezesha wakusanyaji wa mapato ikiwa ni sehemu ya kuwatia moyo ili waweze kukusanya mapato kwa kiasi kikubwa . “ Alibainisha.”


Kwa upande wa Madiwani walitoa shukrani za dhati kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwa kuandaa ziara ya mafunzo ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kupitia vyanzo mbalimbali na namna ya usimaiaji wa miradi ya kimkakati  inayotekelezwa kwenye Halmashauri hizo.

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Mussa Mwanyumbu, Kulia aliyevaa koti jeusi

Mhe. Albert Msando, Mkuu wa Wilaya ya Handeni.

Mhe. John Sallu, Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini, wakwanza kushoto

Ndg. Saitoti Stephen (Wakwanza kulia) Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa