• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Hotuba

HOTUBA YA MHESHIMIWA MKUU WA WILAYA YA HANDENI KWENYE UZINDUZI WA MKUTANO WA UANZISHWAJI WA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI KWA WANAWAKE HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI  TAREHE 20/04/2017   KABUKU.              

Waheshimiwa Viongozi mliopo katika  uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi la Wanawake,  wananchi wote mliohudhuria katika uzinduzi huu, mabibi na mabwana.

Awali ya yote napenda tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutukunisha wote ili kuweza  kuzindua Jukwaa la Uwezeshaji wa Wanawake Kiuchumi la  Halmashauri ya Wilaya ya Handeni hii leo. Kauli mbiu ya siku hii ni “WEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI ILI KUJENGA UCHUMI WA KATI NA TANZANIA YA VIWANDA”.

Ndugu wananchi,

Uanzishwaji wa Majukwaa ya Kuwezesha Wanawake Kiuchumi ni agizo la Mh.Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, ambaye aliteuliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuwa mjumbe mmojawapo  wa timu ya viongozi na wataalam ambao watafanya kazi kama chombo cha juu katika  kupunguza na kuondoa pengo kubwa ambalo limejengeka Duniani na kuongeza ushiriki  wa wanawake katika uchumi duniani kote.  Lengo ni kufikia maendeleo endelevu ambayo pia yamesisitiza uwezeshaji wa wanawake kiuchumi.

Ndugu wananchi 

Mheshimiwa Makamu wa Rais ameelekeza kuwepo na majukwaa ya uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi katika Mikoa yote ikiwa ni pamoja na Halmashauri zake zote za Tanzania. Majukwaa haya yatasaidia kuongeza uelewa wa wanawake katika uchumi, biashara, upatikanaji wa mitaji,  sheria za nchi katika masuala ya uchumi na jinsi ya kujitegemea kiuchumi.

Halmashauri zote zimeelekezwa kuunda majukwaa  kwa ajili ya kuwakutanisha wanawake ili waweze kujadili masuala yao. Sekretarieti ya Mkoa wa Tanga itaratibu shughuli zote za uchumi kwenye Wilaya zote ndani ya Mkoa na kuhakikisha kunakuwa na majukwaa ya Wilaya/Halmashauri zote ambayo yatafanya  vikao vyake kila baada ya miezi sita (6).

                                                                                                              

Ndugu wanachi,

Lengo la jukwaa litakaloundwa ni kukutana pamoja na kujadili fursa, changamoto na jinsi ya kushiriki kikamilifu katika biashara na shughuli nyingine za kiuchumi katika Halmashauri yetu. Vilevile kuongeza uelewa wa wanawake katika upatikanaji wa mitaji, sheria za nchi katika masuala ya  uchumi na jinsi ya kujitegemea kiuchumi.

Wanawake wamekuwa hawapati fursa  za kutosha za kiuchumi hapa Tanzania na hata duniani kote. Hii inatokana na kutokuwa na usawa katika fursa, uwezo wa kupata mitaji na ajira.

Pia jukwaa litasaidia kuondoa matabaka na sheria ambazo zitasaidia kupunguza ubaguzi wa kiuchumi kwa wanawake, ambalo ni jambo la muhimu sana katika kuleta maendeleo ya usawa katika  pato la Taifa, jamii na familia.

Ndugu wananchi,

Nitajisikia fahari sana ndani ya kipindi hiki nikiwa Mkuu wa Wilaya hii ikiwa wataibuka wajasiriamali wakubwa wanawake  miongoni mwenu, nami naahidi kushirikiana nanyi bega kwa bega.

Nimefahamishwa kuwa mtachagua Mwenyekiti wenu wa kwanza kutoka katika mkutano huu wa mwanzo, atakaye simamia malengo yenu hapa Halmashauri, halikadhalika mtaunda pia Sekretarieti itakayohakikisha  kuwa viongozi wa  jukwaa wanatimiza wajibu wao  kwa wakati na kwa haki kwa kufuata sheria zilizopo.

Kazi ya jukwaa mtakaloliunda itakuwa ni kutoa mwongozo wa kimkakati, kuangalia mafanikio ya jukwaa, upashaji habari za kuboresha biashara, kutoa elimu ya kiufundi na mwelekeo kuhusu mitaji na kuweka vipaumbele kuhusu program, fursa za biashara na bidhaa mbalimbali.

Ndugu wananchi, 

Napenda pia kuchukua fursa hii adimu kuwasihi wanawake wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kushiriki kikamilifu katika  vita iliyopo mbele yetu dhidi ya madawa ya kulevya, ukizingatia Halmashauri yetu imepitiwa na barabara kuu ambayo hupitisha  mizigo ya aina mbali mbali kutoka katika sehemu  mbalimbali  za nchi ikiwa ni ndani na nje ya nchi yetu. Natoa rai muwabaini wote wanaojihusisha na  biashara hii haramu wakiwemo wauzaji, watumiaji na wasafirishaji kwa kutoa taarifa kwenye vyombo vyetu vya usalama.

Najua kuna Baraza la Taifa la  Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi kikiwa ni chombo cha juu cha serikali ambacho kilianzishwa ili kuratibu na kuongoza shughuli zote za uwezeshaji wananchi kiuchumi zinazoendeshwa na sekta ya umma na binafsi. Baraza pia linasimamia utekelezaji wa será ya Taifa ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi kwa kuongoza Watanzania  kwenye uchumi imara na  kuhakikisha mazingira mazuri ya biashara na uchumi shirikishi yanakuwepo.

Mwisho natangaza kuwa  leo tarehe 20/04/2017,  Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imezindua  rasmi jukwaa  la uwezeshaji wanawake kiuchumi.

Asanteni kwa kunisikiliza.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa