• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Baraza la Madiwani lampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Imerushwa: November 13th, 2021

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Handeni limefanya kikao chake cha robo ya kwanza cha mwaka wa fedha wa 2021/2022 kwenye ukumbi wa Halmashauri.

Mwenyekiti wa baraza hilo Mhe. Mussa Ibrahim Mwanyumbu ameongoza kikao hicho kwa ajili ya kujadili maswala mbalimbali ya maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

Pia kwenye kikao cha baraza la Halmashauri ya Handeni madiwani walipatiwa semina elekezi ya namna ya kujua majukumu yao kwenye utendaji wao wa kazi. Akitoa semina hiyo Bw. Noel Kazimoto amesema madiwani wanawajibu wa kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo yao, kusimamia ukusanyaji wa mapato, maswala ya elimu, afya, utamaduni na michezo.

Aidha katika baraza hilo lilitoka azimio kuwa kutokana na muundo wa Serikali za mitaa wenyeviti wa vitongoji hawaruhusiwi kumiliki mihuri yeyote kwakuwa hawana mamlaka yoyote ya kupitisha nyaraka zozote kwaniaba ya serikali za vijiji na kwamba Serikali ya kijiji ndiyo ngazi ya pekee ya awali inayoruhusiwa kupitisha nyaraka za serikali.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe.Siriel Mchembe kwenye Baraza hilo alimuagiza meneja wa Mamlaka ya maji vijijini na mijini (RUWASA) kuwa kwenye baraza lijalo watoe taarifa za uchimbaji wa visima vilivyochimbwa na idadi ya visima vinavyotoa maji.

Pia Mhe. Mchembe amesema jumuiaya za watumia maji zina changamoto hivyo madiwani wanantakiwa kutambua nafasi zao kwenye jumuiya hizo na kufahamu matumizi ya fedha zinazipatikana kwa jamii.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Saitoti Zelothe Stephen kupitia baraza hilo ametoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta jumla ya Tsh.1,820,000,000 za UVICO 19 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi wa madarasa katika Shule za Sekondari na Shule Shikizi za Msingi na alisema Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wanayo furaha na heshima kubwa   kwa kuwaletewa fedha nyingi ambazo haizjawahi kutokea kuletwa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa wakati mmoja.

Pia amesema Mapokezi ya fedha hizi zimeleta faraja kubwa sana kwa Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwani zitasaidia kuleta mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia wanafunzi, kupunguza mrundikano wa wanafunzi darasani, kutia hamasa wanafunzi kwenda shule na kupunguza utoro wa jumla na rejareja, kusaidia wanafunzi wa kidato cha kwanza kuanza masomo kwa wakati na vile vile kuwapunguzia mzigo Wananchi katika kuchangia fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa pindi wanafunzi wanapochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza na hivyo kuwasaidia wazazi kujikita zaidi katika maandalizi ya mahitaji ya wanafunzi kwa ajili ya kwenda shule hasa katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka.

Afisa Mipango, takwimu na Ufuatiliaji Bi. Amina amesema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo unakwenda kama ulivyokusudiwa ili kuhakikisha miradi inakamilikia kwa wakati, na kuipa jina la “Kazi iendelee Programme”

Mwisho.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya  Handeni Mhe. Mussa Ibrahim Mwanyumbu, akiongoza kikao cha Baraza hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Siriel Mchembe akiongea kwenye kikao cha baraza hilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Saitoti Zelote Stephen, akiwasikiliza madiwani kwenye kikao cha madiwani.

Wataalam wa Halmashauri ya Handeni wakiwa kwenye kikao cha baraza la madiwani.

Maafisa tarafa wakiwa kwenye kikao.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa