• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI WILAYANI HANDENI LIMERIDHIA RASMI KUACHA KUTUMIA VITABU KUKUSANYIA MAPATO NA KUTUMIA MASHINE ZA EFD TU.

Imerushwa: August 30th, 2017

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Handeni limeridhia kwa pamoja kuacha rasmi matumizi ya vitabu vilivyokuwa vinatumika kukusanyia mapato  kwenye baadhi ya Kata, na kutumia mashine za  kielekroniki  (POS) kuanzia tarehe 1 septemba 2017.

 Makubaliano hayo yamefikiwa leo kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani lililofanyika kwenye ukumbi wa Halmashuri, kufuatia Halmashauri kuongeza  mashine zingine 50 na kufanya jumla ya mashine 80 ambazo zimesambazwa katika kata zote 21.  Mashine hizo zitatumika kukusanyia mapato ambapo kwenye maeneo ambayo yatabainika kuwa na upungufu Halmashauri itaendelea kuongeza mashine.


 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Ramadhani Diliwa amewaeleza Madiwani kwamba, jukumu la kukusanya mapato ni la wote na kila mmoja aone  anawajibu wa kushiriki kuhakikisha anasimamia vyema ukusanyaji wa mapato kwa maendeleo ya Halmashauri. 

 Aliongeza kuwa ukusanyaji wa mapato haujalishi ukubwa au udogo wa Kata, kila Diwani  anao wajibu kuhakikisha vyanzo vya mapato vilivyopo katika eneo lake anavisimamia  ili hata kidogo kilichopo kiweze kupatikana kwa uaminifu wake. Kata zibadilishane mbinu za ukusanyaji wa mapato ili zile zinaoonekana kufanya vyema zisaidie Kata zinazofanya vibaya.

 Aidha Mwenyekiti alimtaka Mkurugenzi Mtendaji  kuhakikisha anafatilia mienendo ya Watendaji  kwa namna wanavyowajibika katika suala la kukusanya  mapato ya Halmashauri na kuboresha pale inapobidi. Watendaji watakaoonekana kwenda kinyume na taratibu hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yao kwa wakati ili iwe fundisho kwa Watendaji wengine.

  Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji  Bw. William Makufwe amewaeleza Madiwani kuwa mashine zimeongezwa ili kuondoa mianya ya ubadhilifu wa mapato ya Halmashuri na kwamba kwa kushirikiana na  wataalamu wa mapato watahakikisha mashine zilizotolewa zinatumiwa kwa malengo yaliyokusudiwa.

 Aidha amewaeleza madiwani kuwa , wataalamu wa mapato na Afisa TEHAMA wataendelea kutoa mafunzo kwa  Waheshimiwa Madiwani kila Kata juu ya matumizi ya mashine hizo ili iwe rahisi kwao kuweza kusimamia vyema ukusanyaji wa mapato kwenye maeneo yao.

 Halmashauriya Wilaya ya Handeni ilianza rasmi kutumia Watendaji wa Kata kukusanya mapato ya ndani kuanzia Septemba 1 mwaka 2016 hadi sasa.

Image may contain: one or more people, people sitting and hat

Image may contain: one or more people, people sitting and indoor 

Baraza la Madiwani likiendelea kwenye ukumbi wa Halmashauri.

  Image may contain: 3 people, indoor

Mwenyekiti wa kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango Mh. Mustafa Beleko akiwasilisha Taarifa

Image may contain: 3 people, people standing and indoor 

Mh. Amina Mnegelo wa Kata ya Kabuku akiwasilisha taarifa ya Tarafa ya Mzundu

Image may contain: 2 people, indoor 

Mwenyekiti wa Kamati ya Ukimwi Mh. Abdalla Pendeza akiwasilisha taarifa wakati wa baraza.

Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Mh. Joel Mabula akitoa taarifa kwenye kikao cha Baraza .

Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe akizungumza kwenye baraza lililofanyika leo.



Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa