• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Buku Tano, Tiba mwaka mzima

Imerushwa: July 20th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh Godwin Gondwe amewataka wananchi wilayani Handeni mkoani Tanga kujiunga na mfuko wa bima ya matibabu (CHF) iyoboreshwa ambapo kwa shilingi elfu 30, jumla ya watu 6 kutoka kwenye familia moja watapatiwa matibabu kwa kipindi cha mwaka mmoja katika zahanati, hospitalina vituo vya afya vyote ndani ya mkoa wa Tanga.

Akiongea wakati wa kufungua Kampeni maalumu ijulikanayo kama *BUKU TANO,TIBA MWAKA MZIMA* iliyofanyika katika viwanja vya shule ya Msingi Kabuku nje, DC Gondwe amesema kuwa gharama ya shilingi elfu 30 kwa watu sita ni sawa na kila mmoja kulipia shilingi 5000 na kupatiwa matibabu mwaka mzima.

Aidha Mh. Gondwe amewataka watumishi wa zahanati, vituo vya afya pamoja na Hospitali ya wilaya kutoa kipaumbele kwa wananchi wenye bima za afya pindiwanapokwenda kupata huduma hizo za afya.

Pia katika ufunguzi wa kampeni hiyo Mh.Gondwe aligawa simu janja 43 kwa Watendaji wa Vijiji kwa ajili ya kusajili wanachama wa bima ya matibabu (CHF) iliyoboreshwa ambapo wakishasajiliwa taarifa zao zitasoma moja kwa moja kwenye mfumo wa CHF iliyoborehwa

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe amefafanua kwa kusema kuwa, Serikali ilifikia maamuzi ya kupanua wigo mpana wa bima ya matibabu (CHF) ili kutoa fursa kwa wananchi kutibiwa mahali popote ndani ya mkoa wa Tanga huku akimshukuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa kuwezesha wananchi kupata
huduma bora za afya kwa muhstakabali wa maisha yao.

Nao baadhi ya wananchi ambao wamejiunga na bima hiyo ya matibabu (CHF) iliyoboreshwa wameeleza namna ambavyo bima hiyo imewasaidia ambapo wamesema kuwa wamekuwa wakipatiwa huduma bora za afya na hivyo kutoa wito kwa wengine kujiunga na bima ya matibabu (CHF) iliyoboreshwa."Ugonjwa haupigi hodi na kama unamiliki kadi ya bima hauta kuwa na wasiwasi", alisema mnufaika Mwanahamis Salum.

Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya bima ya matibabu  (CHF) iliyoboreshwa Mganga mkuu wa wilaya ya Handeni Dk Credianus Mgimba amesema kuwa Mpaka sasa tayari kaya 130 zenye jumla ya wanufaika wa bima ya matibabu (CHF) iliyoboreshwa 772 wameshajiunga  huku lengo likiwa ni kupata kaya 52303.


MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Gondwe akimpatia simu janja moja ya watendaji kwaajili ya kusajili wanachama wa CHF


Mkurugenzi wa Handeni Bw. William Makufwe akimptia simu janja moja ya watendaji kwaajili ya usajili wa wanachama wa CHF


Viongozi mbalimbali walitoa simu kwa watendaji kwaajili usajili wa wanachama wa bima ya matibabu (CHF).


Mnufaika wa bima ya CHF akiwa kwenye picha ya pamoja na Mh.Gondwe

Mganga Mkuu Wilaya ya Handeni Dr.Credianus Mgimba kushoto akiwa kwenye picha ya pamoja na Mh.Diwani wa Kata ya Kabuku nje Amina Mnegelo

Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala wa kulia Bi.Fatuma Kalovya akiwa kwenye picha ya pamoja na Mh. Gondwe

Mkuu wa Idara ya Mipango Bi. Edina Katalaiya kulia akiwa kwenye picha ya pamoja na Mh.Gondwe

Wadau mbalimbali walishiriki katika ufunguzi wa kampeni ya Buku Tano, Tiba mwaka mzima.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa