• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CDMT yaboeresha miundombinu ya vyoo Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

Imerushwa: February 22nd, 2018

Uongozi wa Halmashauri ya Wilayaya Handeni umekabidhiwa rasmi mradi wa choo cha matundu sita kilichojengwa na shirika lisilo la Kiserikali CDMT(Community Development Mission of Tanzania) lenye thamani ya Milioni 19 za Kitanzania  kwa lengo la kuboresha huduma ya vyoo kwa wanafunzi wa shule za Msingi.

Akipokea mradi huo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bw. Aweso Bakari ( Afisa Tarafa Mkumburu) alisema kuwa anashukuru sana CDMT kwa kuona uhitaji wa Shule ya Masatu na kuamua kusaidia ujenzi wa choo chenye  matundu 6 yatakayosaidia kupunguza changamoto ya vyoo shuleni hapo.

Kaimu Mkurugenzi alisema kuwa,Shule ya Masatu kwa mujibu wa ripoti ya Mwalimu Mkuu ilikuwa na upungufu wa matundu 29 ya vyoo, Hivyo kwa mradi wa matundu 6 yaliyojengwa na Shirika la CDMT umepunguza na kufikia matundu 23, hivyo  anashukuru Shirika hilo  kwa jitihada za kuunga Mkono Serikali katika ujenzi wa miundombinu.

Aidha aliwataka viongozi wa shule na Kijiji kuhakikisha wanatunza mradi huo kwa kuzingatia usafi wa mazingira ili hata waliofadhili mradi huo wakija kuutazama wafarijike na waweze kuisaidia Serikali kutatua changamoto nyingine ambazo bado zinaikabili shule hiyo.

“Naishukuru sana CDMT , Viongozi wa shule na Kijiji msimamie mradi huu vizuri kuhakikisha hauharibiwi kwa michoro ya ajabu na usafi uzingatiwe ili hata wafadhili wakija kutembelea waone thamani yake” alisema Aweso

Kwaupande wake Diwani wa Kata ya Segera Mh. Yassin Mtamike alisema kuwa, anaishukuru CDMT na yeye kama Diwani atahakikisha mradi huo unatunzwa na kulindwa ili kuwapa nafasi wafadhili waweze kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutatua changamoto mbalimbali za miundombinu.

Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali CDMT(Community Development Mission of Tanzania) na Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Emile Philipo alisema kuwa baada ya kufika Handeni aligundua changamoto ya vyoo bora kwa Shule za Msingi na kuamua kuandika andiko la kuomba msaada kwa Serikali ya Marekani yenye fungu la fedha la Rais wa Marekani linalosaidia Afrika kwa lengo la kupunguza changamoto ya vyoo.

 Aliongeza kuwa kwa tafiti zake  za awali aliamua kusaidia shule tatu za msingi ambapo shule  2 za Msomera na Masatu zipo Hamashauri ya Wilaya ya Handeni na shule moja  1 ya Seuta Halmashauri ya Mji Handeni.

Miradi yote imekamilika kwa jumla ya Milioni 58 za Kitanzania ambapo kila shule imejengewa matundu 6 ikiwa matundu 3 kwa  wanafunzi wa kike na 3 kwa wanafunzi wa kiume.

Muonekano wa  jengo la choo kwambele.

Muonekano wa jengo la choo kwa nyuma


ukaguzi wa mradi ukiendelea kabla ya makabidhiano.

Viongozi wakikagua mradi kabla ya makabidhiano

Diwani wa Kata ya Segera Mh.Yassin Matamike kulia  akimshukuru Mkurugenzi wa CDMT Bw. Emile Philipo  kwa kupena mikono wakati wa makabidhiano ya mradi huo.

Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Masatu Bw. Daniel Daniel akishukuru kukabidhiwa kwa mradi vyoo vya wananfunzi shuleni kwake na Mkurugenzi wa CDMT na Afisa Ushirika Wilaya Bw.Emile Philipo.

Mtendaji wa Kata ya Segera  Kulia Bi.Rukia Aweso akipeana mkono wa Shukurani na Mkurugenzi wa CDMT kushoto Bw. Emile Philipo.

Picha ya pamoja baina ya Viongozi, Mkurugenzi wa CDMT na uongozi wa Halmashauri ya Kijiji cha Masatu mara baada ya kukabidhiwa rasmi jengo la vyoo.

muonekano wa choo kwa ndani.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bw.Aweso Bakari aliyenyoosha mkono akitoa shukurani kwa ujenzi wa jengo la choo hicho.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa