• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CETA yafanya tahmini Handeni DC

Imerushwa: December 12th, 2018


Taasisi isiyo ya kiserikali inayosimamia maswala ya utawala bora vijijini inayoitwa Civil Education Teachers Association (CETA)  imefanya kikao cha  tahmini ya kamati zake za vijiji leo katika Ukumbi wa Neema ulioko katika Kata ya Mkata ambapo tahmini hiyo hufanyika kila mwisho wa mwaka ili kuona utekelezaji wa kazi walizofanya, mafanikio na Changamoto .

Akifungua kikao hicho kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bi.Fatuma Kalovya aliwaeleza wajumbe kuwa serikali inaipongeza shirika la CETA kwa mchango mkubwa wanaoutoa katika kuleta maendeleo katika jamii na pia kuipa mafunzo kamati zilizochaguliwa kwenye vjiji mbalimbali ili kufanya ufuatiliaji wa maswala ya utwala bora kwa ufanisi.

Aidha alishukuru kamati hizo kwa kufuatilia miradi mbalimbali inayoendelea na kutoa taarifa na kwamba kupitia taarifa hizo,  mambo maovu yanayoendelea vijijini  yamekuwa yakichukuliwa hatua. Pia aliwaambia wasijikite kwenye shughuli za maendeleo tu lakini waangalie na mienendo ya kazi za watumishi wa serikali na pale inapotokea baadhi ya watumishi hawatimizi majukumu yao ipasavyo wasisite kutoa taarifa.

Aliongeza kwa kuwaambia wanakamati hao kuwa kazi wanayofanya ipo kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria hivyo waifanye kwa ujasiri na kwa kujiamini kwani serikali inathamini kazi yao na inawaahidi kuwalinda na kwamba kamati yoyote ikipata usumbufu ipeleke malalamiko yake  Idara ya maendeleo ya jamii kitengo cha dawati la malalamiko madai hayo yatashughulikiwa kwa wakati.

Pia amewasihi wanakamati hao kuendelea kutoa elimu kwa wananchi na viongozi kupitia mafunzo waliyofanyiwa kwani suala la utawala bora bado ni changamoto katika ngazi za vijiji kwasababu mikutano ya vijiji havifanyiki kwa wakati na maeneo mengine havifanyiki kabisa kitu kinachofanya maendeleo yarudi nyuma hivyo watoe elimu ili vikao hivyo vifanyike kwa wakati na kwa mujibu wa ratiba iliyowekwa.

Kalovya aliwaeleza pia kamati hizo kutumia maafisa maendeleo ya jamii ili waweza kuwasaidia katika suala la uhamasishaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo na kuhamasisha vikao kwani bila vikao wananchi hawawezi kuchangia shughuli za maendeleo lakini pia wananchi hawataweza kupata mrejesho wa michango yao waliyotoa hivyo wanakosa imani na viongozi  wao hata kama hakuna lolote baya limefanyika “bila vikao vya mapato na matumizi wataona wanaibiwa hata kama hakuna kitu”alisema.

Alihitimisha kwa kuwataka kushiriki kwa pamoja kuhakikisha rasilimali za umma zinatumika kwa manufaa ya umma hasa masuala ya uuzwaji holela wa ardhi bila kufuata sheria hivyo wasisite kutoa taarifa kwani ofisi ziko wazi, Pia aliomba uongozi wa CETA kupatia mafunzo kamati za vijiji vilivyobaki kwakuwa mpaka sasa wamewapatia mafunzo wanakamati wa vijiji 44 kati ya vijiji 91.

Mkurugenzi wa CETA Bw. Safari Minja alisema shirika hilo limenza kufanya kazi Tanzania tangu mwaka 2003 lakini kwa Handeni ilianza kufanyakazi mwaka 2012 ambapo ilianza na mafunzo ya wanakamati katika vijiji 9 na kadiri muda unavoenda walizidi kuwaongeza hadi kufikia vijiji 44 mwaka huu na kwamba lengo lao ni kufikia vijiji vyote 91 vya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni ifikapo mwaka 2020.

Alisema baada ya  kamati hizi kufanyiwa mafunzo ya wajibu na majukumu ya serikali za vijiji na kuanza kufanya ufuatiliaji ubadhirifu wa fedha za serikali umepungua kwani wamekuwa wakitoa taarifa na hatua mbalimbali zilichukuliwa lakini pia miradi iliyosimama ilitekelezwa na kutumika na jamii kwa matumizi yaliyokusudiwa, taratibu za matumizi ya fedha zimetumika na kwa wale viongozi wanaokusanya fedha bila risiti pia wamedhibitiwa na sasa fedha zinakusanywa na risiti halali za Halmashauri zinatolewa.

Moja wa wanakamati ya kufuatilia maswala ya utwala bora vijijini Bw.Hassani Selemani alisema kupitia shirika hili tumepata elimu juu ya utawala bora kwani mwanzo tulikuwa hatuelewi na sasa tunauelewa mkubwa  na pia tunafuatilia na kulinda ya rasilimali za serikali  ili zitumike kwa maslahi ya umma lakini pia vitumike vizuri.

Aidha alisema changamoto wanazokutana nazo ni baadhi viongozi kutokuwa wawazi kwao pale wanahitaji maelezo kuhusu jambo na pia hawataki kukaguliwa au kuwazungusha pale wanapohitaji taarifa.

Baada ya kikao hicho kamati za vijiji vilivyofanya vizuri walipewa zawadi ya baiskeli kwa kila kijiji kama ambavyo wao wenyewe waliomba kupewa hizo baiskeli ambapo vijiji hivyo vilikuwa 6 ikiwepo kijiji cha Kitumbi, Manga, Magamba, Kwamatuku, Kibindu na Mazingara lakini pia Mwenyekiti wa wanakamati Halmashauri ya Wilaya alipewa simu janja(smart phone).


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bi.Fatuma Kalovya akizungumza


Wajumbe wakisikiliza maelekezo

Wanakamati wakiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi baada ya kukabidhiwa baiskeli na mwenyekiti wa wanakamati Wilaya alipewa simu janja

Timu ya viongozi kutoka Halmashauri wakiwa kwenye picha ya pamoja 

Kamati pia zilisoma majukumu waliyotekeleza kwa Mkurugenzi kipindi cha mwaka mzima.

Mkurugenzi wa CETA Bw.Safari Minja akizungumza katika kikao hicho.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa