• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC Gondwe afanya kikao kazi na wadau wa elimu na afya

Imerushwa: December 3rd, 2019


Kikao hicho kilifanyika jana katika ukumbi wa CCM Halmashauri ya mji Handeni ambapo kilihudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwepo Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Handeni,Wakurugenzi watendaji, Viongozi wa dini, Waheshimiwa madiwani, Wataalam wa Halamashauri ya Mji Handeni na Wilaya ya Handeni, Maafisa Tarafa, Watendaji Kata, Maafisa elimu Kata, wakuu wa shule na walimu wakuu.

Akizungumza katika kikao hicho Mh. Godwin Gondwe ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni amesema lengo la kikao hicho ni kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayofanya lakini pia kuwakumbusha wadau hao namna ya kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Mh. Gondwe  amewataka viongozi wa Idara ya Afya kuhakikisha wanaandika dawa zote muhimu kwenye mbao za matangazo katika zahanati na vituo vya afya ili wagonjwa waweze kujua na amesema hii itasaidia wagonjwa wanaotumia kadi za bima ya matibabu iliyoboreshwa (ICHF) wasilalamike huku akiwataka Watendaji Kata kukagua kama orodha ya dawa hizo zimeandikwa.

Pia aliwataka Waganga wakuu kuhakikisha huduma ya kuandikisha wananchama wapya wa bima ya matibabu iliyoboreshwa (ICHF) inafanyika bila kusimama hii ni baada ya wadau kulalamika kutokuwepo kwa  huduma hiyo katika baadhi ya maeneo na kwamba zile Kata ambazo bado hazijazindua kampeni ya bima ya matibabu iliyoboreshwa wanafanya ndani ya mwezi moja

Aidha Gondwe amewamesihi wadau kushirikiana kupiga vita mimba na ndoa za utotoni ili watoto hao wa kike kufikia ndoto zao na amesema takwimu za mimba zipelekwe kila mwezi pamoja na  kesi zote ambazo ziko ngazi ya Kata na vijiji wahakikishe wamepeleka ngazi ya Wilaya hii ni baada ya viongozi wa Idara ya elimu kusoma taarifa na kuonyesha kesi nyingi kuwa ngazi za vijiji na Kata kwa mda mrefu.

Alihitimisha kwa kuwataka Wakuu wa shule kuhakikisha wanafunzi wanaongea kiingereza hii baada ya kutembelea baadhi ya shule na kukuta wanafunzi hawajui kuongea lugha hiyo hivyo amewaekelekeza Wakuu hao wa shule wanafunzi kutokuongea lugha zingine wakiwa shule na kufanyika kwa midahalo mbalimbali kwa lugha ya kiingereza ili wanafunzi wajifunze kuongea lugha hiyo na kwamba hiyo itasaidia ufaulu kuongezeka.

MWISHO

Imeandaliwa na;

Paulina John

Kitengo cha Habari na mawasiliano Handeni DC

Mh.Godwin Gondwe akizungumza na wadau elimu na Afya

Katibu Tawala wa Wilaya ya Handeni Mwl. Boniphace Maiga akitoa neno la nasaha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe akizungumza


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Handeni akizungumza

Wataalam wa Idara ya afya Halmashauri ya Wilaya na Mji Handeni wakisoma taarifa za shughuli walizotekeleza

Watalaamu wa Idara ya Elimu Halmashauri ya Wilaya na Mji Handeni wakisoma taarifa za maendeleo ya elimu

Viongozi wa dini wakitoa ushauri ili Wilaya ya Handeni ifikie malengo yake

Wadau wakifuatilia mazungumzo ya kikao

Wadau mbalimbali wakiuliza maswali na kutoa ushauri






Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa