• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ELIMU YA SHERIA IZIDI KUTOLEWA KUWAPA WANANCHI UELEWA WA NAMNA YA KUSHUGHULIKIA KESI ZAO.

Imerushwa: February 1st, 2018

Katika kuhitimisha juma la sheria muwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni Bi. Upendo Magashi (Afisa Tawala Wilaya) amewaasa wanasheraia na watumishi wa mahakama kuendelea kuelimisha wananchi mambo mbalimbali yanayohusu sheria ili kurahisisha upatikanaji wa haki.

Rai hiyo imetolewa leo alipokuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mh. Gowin Gondwe kwenye maadhimisho ya kilele cha juma la sheria yaliyofanyika kwenye  viwanja vya Mahakama ya Wilaya. Alisema wananchi wengi wakishindwa kesi wanaenda kulalamikkia kwenye maeneo yasiyostahili wakijaribu kutafuta msaada.

Afisa Tawala amesema ni vyema wananchi wakajua taratibu na kanuni za kufuata tangu kesi inapoanza hadi tamati ili kuwasaidia kuweza kupata haki zao na kuepuka malalamiko yanayoweza kuzuilika.

“ Ni imani yangu kwamba kila muhimili ukifanya kazi kwa weledi , malalamiko yatapungua na wananchi wataweza kujishughulisha na shughuli nyingine za maendeleo. Matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano yanalenga kuboresha utoaji wa huduma hivyo tutumie ipasavyo” alisema Afisa Tawala

Ameongeza kuwa  katika kipindi ambacho Teknolojia inakua  mazingira ya kazi na vitendeakazi lazima vibadilike kulingana na wakati  ili kuweza kukidhi  mahitaji ya wananchi, Na kuendelea kuzingatia maadili na weledi ili kila mmoja aweze kupata haki kwa wakati.

“Mbali na changamoto zilizopo Serikali inaendelea kuziba mapengo yaliyopo na kuhakikisha upatikanaji wa vitendea kazi vitakavyosaidia usikilizaji wa kesi na utoaji wa nakala za hukumu kwa wakati, Hivyo Watumishi wa Mahakama wanapohitaji kwenda kupata mafunzo mafupi waruhusiwe ili waweze kwendana na kasi ya matumizi ya TEHAMA” amesema Afisa Tawala.

Aidha aliwataka waendesha mashitaka na wapelelezi kuhakikisha wanawapa wafungwa muendelezo wa kesi zao badala ya kuwaacha wakiwa hawajui  hatma ya kesi zao.

Naye muwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Dk.Philis Nyimbi (Katibu Tawala Kilindi) amesema uwepo wa muhimili  wa Mahakama  umewezesha viongozi kuweza kufanya kazi kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa,  Hivyo kwa kutumia TEHAMA kutawezesha kupata taarifa sahihi za washtakiwa kwa wakati na kutoka mahakama moja kwenda nyingine.

Mh. Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Handeni na Kilindi  Bw.Anorld Kileo amesema kuwa  maadhimisho ya juma la sheria huashiria mwaka  mpya wa Mahakama,  ambapo  inapata nafasi ya  kujitathmini kiutendaji na kuweka malengo na mikakati inayotekelezeka  kwa mwaka mwingine.

Ameongeza kuwa Mahakama inalenga kutoa elimu pana kwa jamii na, kwakutumia TEHAMA Mahakama itaweza kutekeleza kwa weredi jukumu la msingi la utoaji haki, kuimarisha uwazi na uwajibikaji, kusikiliza na kutatua kero za wananchi ili kuhakikisha inakua sehemu pekee ya watu kupata haki.

Maadhimisho ya siku ya sheria Nchini  hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza ya mwezi wa pili. Maadhimisho hayo yalijumuisha wadau  mbalimbali kutoka Wilaya ya Handeni na Kilindi , wakiwemo Wanasheria, Mawakili, Idara ya Uhamiaji, Magereza, TAKUKURU na Polisi, yenye kauli mbiu ya  “Matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa haki kwa wakati na kwa kuzingatia maadili”.

Muwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni Bi. Upendo Magashi  (Afisa Tawala Wilaya)  akihutubia wananchi kwenye kilele cha juma la sheria.

Dk Philis Nyimbi muwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mh. Sauda Mtondoo  akizungumza kwenye kilele cha juma la Sheria.

Mh. Anorld Kileo   Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Handeni na Kilindi   akizungumza na wageni waalikwa na wanachi kwenye kilele cha juma la Sheria

Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw.Amani mangesho akitoa maada kwenye kilele cha juma la Sheria.

Meza kuu

Mwanasheria wa Halmashauri ya Mji Handeni Mwanaamina Mruma akizungumza na wanachi kwenye maadhimisho ya kilele cha juma la Sheria

Baadhi ya wananchi

Mkuu wa Takukuru Wilaya ya Handeni Bi. Esta Mulima  akisisitiza kuzingatia maadili ili kuepusha vitendo  vinavyoweza  kusababisha lengo la kutoa haki kwa wakati lisitimie Kama ilivyokusudiwa.

Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya Handeni

Habib Rashid (moja kwa moja)  kutoka Ithnasharia Community akiomba wananchi wafahamishwe juu ya sheria na taratibu za kufuata pale ambapo hawajaridhia na hukumu iliyotolewa.

Picha ya pamoja Mara baada ya maadhimisho

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa