• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya Wilaya ya Handeni yapata mwekezaji wa madini ya Dolmite

Imerushwa: July 19th, 2018


Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe amekutana  na wawekezaji wa madini ya DOLMITE kutoka India  lengo likiwa ni kutembelea maeneo  yenye madini hayo ili kuona wingi na ubora ambapo walitembelea moja ya maeneo hayo katika kijiji cha Chanika Kofi Kata ya Ndolwa.

Akizungumza na wawekezaji hao jana Mh. Godwin Gondwe aliwapongeza na kuwashukuru kuja kuwekeza Handeni na pia aliwahakikishia kuwa madini ya DOLMITE yapo ya kutosha Handeni kwa kuwa kuna hekta nyingi za maeneo mbalimbali yenye madini hayo hivyo watapata malighafi ya kutosha na yenye ubora kulingana na mahitaji ya kitu wanachohitaji kutengeneza na kwamba kuwekeza kwao Handeni ni moja ya kutimiza ndoto ya Mh.raisi ya Tanzania ya viwanda.

Aliongeza kwa kusema kuwa sera ya serikali ya Tanzania inawaunga mkono wawekezaji hivyo kwa msaada wowote watakaouhitaji yeye yuko tayari kuwasaidia na pia kwa kuwa malighafi mengi yanapatikana Handeni hivyo kiwanda pia kitajengwa Handeni ni kiasi cha kuchagua sehemu bora ambayo itakidhi mahitaji ya kuendesha kiwanda hicho.

Amehitimisha kwa kuwataka wananchi  kuwapokea wawekezaji hao na kuwapa mazingira bora ya kuwekeza na kwamba  Handeni ajira za kudumu na muda zitapatikana  kupitia wawekezaji hao hivyo maafisa biashara na idara ya maendeleo ya jamii kuhakikisha wawekezaji wakija wanahudumiwa haraka ili wawekeze haraka, serikali ipate kipato chake na wao kama wawekezaji waweze kunufaika na uwekezaji wao katika nchi yetu ya Tanzania.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmasahuri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe amewashukuru wawekezaji  hao kuonyesha nia ya kuja kuwekeza Handeni  na kwamba Handeni inawakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza katika sekta mbalimbali  kwani Handeni inamikakati ya kuhakikisha kwamba wawekezaji wakifika kwenye Wilaya yetu na wamevutiwa na uwekezaji wowote tunawapa ushirikiano  unaostahili kwa kuwa nia yetu ni kutengeneza viwanda vingi kadiri inavyowezekana ili kufikia nia na ndoto ya Mh.raisi wetu ya kutengeneza viwanda vyenye thamani ya mahitaji yetu tuliyonayo

Kwa upande wake kaimu Afisa madini mkazi wa Wilaya ya Handeni Bw.Naiman Abdiel Samana aliwaeleza wawekezaji hao kuwa Handeni ina aina mbalimbali ya madini yakiwepo madini ya viwandani, madini ya ujenzi na madini ya vito ambayo yanapatikana katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Handeni, Pia kwa upande wa madini ya Dolomite Handeni ina jumla ya hekta 302.69  yakiwepo maeneo ya Kwedikwazu,Chanika Kofi na Mumbwi na maeneo hayo yanafikika kwa urahisi na kwamba wao wakotayari kuwaelekeza wawekezaji  namna ya kupata leseni ya utafiti na leseni ya uchimbaji wa madini.

Naye mkazi wa kijiji cha Chanika Kofi BW.Hassani Mkombozi  amesema kuwa amefarijika kuona ujio wa wawekezaji   kwani wanahandeni watanufaika kupitia wawekezaji hao kwa kupata ajira zitakazoinua hali ya uchumi ya watu wa Handeni.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa