• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imepokea miche ya mikorosho 140000

Imerushwa: April 13th, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imepokea miche 140000 kutoka Bodi ya Korosho na kugawiwa kwa wananchi bure kama zao biashara ili wananchi waondokane na umaskini kwani kwa miaka mingi zao kuu kwa Handeni lilikuwa mahindi.

Ambapo wananchi waliuza mahindi hayo kupata kipato cha kujikimu kitu kinachowasababishia kukosa chakula hivyo mwaka 2016/2017 viongozi wa Wilaya walitafuta mbinu mbadala ya wananchi kujikwamua kiuchumi  kwa kuchagua mazao mawili ya biashara ambayo ni zao Mhogo na Mikorosho na zao Mhogo lilifanikiwa kwa asilimia zaidi ya 70 kwani wananchi wamelima kwa wingi na kupata mafanikio.

Akizungumza katika  uzinduzi wa upandaji  wa Mikorosho ulioambatana na juma la upandaji miti uliyofanyika  Katika Shule ya Sekondari Mazingara  na baadaye katika  Kijiji cha Mkata Mashariki jana , Mkuu wa mkoa wa Tanga Mh.Martin Shigela ambaye aliwakilishwa na  Mh.Godwin  Gondwe  Mkuu wa Wilaya ya Handeni  amesema wameamua kuleta zao la korosho kama zao mbadala la biasahara kwa wananchi wa Handeni ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Mgeni rasmi amewaeleza wananchi kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni mpaka sasa imepanda miche 20,000 ya mikorosho na leo imepokea miche 140000 na lengo letu nikufikia miche 300,000  ili wananchi waondokane na umaskini  na pia kujipatia kipato cha muda mrefu na  aliwaeleza  wananchi  malengo  madhubuti ya kuanzisha zao hilo la Korosho kuwa ni kuendana na mabadiliko ya tabia ya nchi kwamba kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa hivyo hatupaswi kulima mazao yanayostahimili ukame ili waondokane na adha ya kukosa chakula na kipato cha kukimu mahitaji yao.

Lengo lingine ni kuongeza na kuinua uchumi wa mwananchi moja moja kwamba mtu akiwa na shamba la korosho ataondokana na umaskini kabisa kwani atakuwa na maisha mazuri kwa kujenga nyumba nzuri,atasomesha watoto na atapata fedha za matibabu alisema” uzinduzi huu wa kilimo cha korosho maana  ni kwamba umaskini kwaheri”

Pia amesema lengo lingine la kulima zao hilo ni kuongeza mali ghafi katika viwanda vyetu kwani anayezalisha mali ghafi ni mkulima  na moja wa wakulima hao ni wakulima wa Handeni hivyo aliwaasa wananchi kusimamia matumizi na umiliki wa bora ya ardhi kwaajili ya uzalishaji wa mali ghafi hizo kwani  baadhi yao wamekuwa chanzo cha migogoro ya ardhi na pia baadhi yao wamekuwa chanzo cha uuzaji wa ardhi kiholela hivyo wananchi wahahkikishe wanaunga mkono upandaji wa korosho kwa kasi ya Mh.Raisi. Aidha aliwashukuru askari JWTZ kutoka kitengo cha magari na usafirishaji makao makuu  Dres-salaam kwa kuonyesha uzalendo wao kwenda kufuata miche hiyo ya mikorosh na pia kutoa malori yao bure kwaajili ya kubeba miche hiyo  pia aliwapongeza  viongozi wa Handeni na wananchi wote kwa kuunga mkono zoezi hilo la kuanzisha mazao ya biashara.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  Mh.Ramadhani Diliwa amesema kuwa wananchi wa Handeni kwa miaka mingi wamekuwa wakilima zao moja la mahindi ambapo zao hilo halikutosheleza mahitaji yao na kuishi kwa mikopo ya kudumu kwani wakivuna wanalipa madeni na kuendelea kukopa hivyo aliwataka wananchi kutumia ardhi  waliyojaliwa na mwenyezi Mungu  kwani Handeni ina ardhi ya kutosha na kama sisi wakulima kipato chetu ni kilimo turudi kulima  mazao ya uchumi  kama Mihogo,Korosho,Michungwa,miembe  mazao mabayo yanadumu zaidi ya miaka 50 aliesma”Tulimeni mazao ya biashara”.Amesema pia tunafanya hivyo ili Halmashauri ipate mapato ya ndani ya kutosha ambayo yatatumika kuwahudumia wananchi .

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe amewataka wananchi kuwa na utayari wa kilimo hicho cha korosho na kwamba hata kama miche hiyo itagawiwa bure lakini lazima anayepewa miche hiyo ataingia mkataba na Halmashauri kukiri kupokea na kuitunza kwa muda wote na endapo hataitunza  miche hiyo   atalipa fidia kwa kulipa shilingi 500 kwa kila mche hivyo kila mtu aelewe kuwa hatutoi miche hiyo kiholela  lazima mtu awajibike kwa miche tuliyomkabidhi ili tuwe na uhakika wa miche kukua vizuri na kutunza na kwa upande Kata miche hiyo itakabidhiwa kwa watendaji Kata hivyo wasimamie ugawaji huo kwa wananchi na pia kusimamia maendeleo yake.

Amesema  mwakani tutaongeza miche zaidi ya mara tatu ya mwaka huu  ili wananchi wawe na maisha mazuri kwa kujenga nyumba nzuri,wasomeshe watoto na pia kukidhi garama za matatibabu pale wanapougua. Pia amewaasa viongozi na Waheshimiwa madiwani kuw wakirudi  katika maeneo yao wawahamasishe wananchi kuwa miche ya mikorosho ipo hata kwa kuknunua  waweze kupanda kwa wingi ili waondokane na hali duni ya kipato.

Pia  Ofisa Kilimo,Uvuvi na Umwagiliaji  wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw.Yibarila Chiza ameelezea mikakati ya kuendeleza kilimo cha Korosho kwa kusema kuwa Halmashuri imelenga kuongeza maeneo ya uzalishaji wa zao la korosho katika msimu wa mwaka 2018/2019 kiasi cha ekari laki moja  kutarajiwa kupandwa miche ya mikorosho ambayo ni  mara tatu ya msimu huu.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa