• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI YAFUNGUA STOO/DUKA LA DAWA KUKABILI CHANGAMOTO YA UPUNGUFU WA DAWA.

Imerushwa: June 12th, 2017

Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imefungua duka/stoo ya kuhifadhia dawa ili kukabiliana na changamoto ya upungufu na ukosefu wa dawa kwa wakati kwenye Hospitali ya Wilaya ya Handeni.

Uwepo wa duka hilo umekuja kufuatia changamoto zilizokuwa zinaikabili Hospitali pamoja na Vituo vya Afya  ya upungufu na ukosekanaji wa dawa na wakati mwingine kutokupata dawa kwa wakati pindi wanapoagiza Bohari Kuu ya Dawa (MSD).

Akizunguma Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni BW. William Makufwe wakati wa ziara na madiwani kwenye Duka/ Stoo hiyo alisema kuwa, tumeamua kukabiliana na changamoto ya upungufu na malalamiko ya wananchi ya ukosefu wa dawa kwa muda mrefu kwenye Hospitali yetu na vituo vya afya kwa kufungua Duka/Stoo ambayo itakuwa na dawa za aina mbalimbali ili kuboresha huduma.

Aliongeza kuwa vituo vyote vya afya kwasasa vitakuwa vinachukua dawa kwenye duka/stoo  ya Hospitali ya Wilaya pindi dawa zinapohitajika badala ya kuagiza moja kwa moja MSD.

kuagiza dawa MSD kulikuwa kunachelewesha upatikanaji wa dawa kwa wakati na hivyo kusababisha upungufu wa dawa ambao ulikuwa unasababisha malalamiko ya muda murefu kutoka kwa wananchi.

“ukiona unapata maelezo yasiyoeleweka kuhusiana na upatikanaji wa dawa kwenye maeneo yote yanayotoa huduma za afya piga simu kwangu moja kwa moja namimi nitashughulikia” alisema Makufwe.

Aidha, aliwaomba waheshimiwa madiwani kuendelea kuhamasisha kaya kuendelea kujiunga na mfuko wa  afya wa jamii (CHF) ambao kwa kiasi kikubwa umesaidia upatikanaji wa fedha za kununulia dawa, ambapo kwa kuongeza idadi ya kaya wanaojiunga na CHF kutasaidia kuwepo kwa dawa maratatu zaidi ya zilizopo.

 Aliwaomba pia kusimamia dawa zinazopelekwa kwenye vituo vyao vya afya ili  kuepuka dawa kuhujumiwa na kuibwa.

Mfamasia wa Hospitali ya Wilaya ya Handeni Mustafa Lutavi alisema kuwa kabla ya kufunguliwa kwa duka hilo hospitali ilikuwa inachangamoto kubwa ya ukosefu wa dawa za kutosha hali iliyopelekea malalamiko ya mara kwa mara kwa wananchi wanaopata huduma kwenye hospitali hiyo na vituo vya afya.

Alieleza kuwa CHF imepanga kuboresha huduma zake ambapo badala ya wananchama kupata huduma kwenye vituo vilivyopo Wilayani, waanze kupata huduma ngazi ya Mkoa.

Mbunge wa Handeni Vijijini Mh. Mboni Mhita na waheshimiwa madiwani walimpongeza Mkurugenzi na timu yake nzima kwa ujumla kwa jitihada walizozionesha katika kukabiliana na changamoto hiyo na kwamba wao kama viongozi wenye dhamana kwa wananchi wataendelea kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa afya wa jamii CHF ili kuendelea kuboresha huduma za Afya, huku akiahidi kuendelea kufuatilia uapatikanaji wa watumishi wa idara ya afya kupunguza changamoto ya upungufu wa watumishi.

Baadhi ya Waheshimiwa Madiwani wakiwa kwenye duka la dawa.

Baadhi ya Dawa


Waheshimiwa madiwani wakiwa kwenye picha ya pamoja nje ya Duka/Stoo ya Dawa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa