• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Handeni DC yakabidhi Madarasa ya UVIKO-19 ndani ya Muda.

Imerushwa: December 19th, 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Saitoti Zelothe Stephen ameogonza Halmashauri hiyo kukabidhi vyumba 91 vya madarasa kwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni  yaliyojengwa kwa fedha za UVIKO-19 kwa shule za Sekondari na shule shikizi vilivyokamilika kwa asilimia 100% .

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Siriel Mchembe amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajali wananchi wanyonge kwa vitendo kwa kuipatia Halmashauri ya Wilaya  ya Handeni fedha kwaajili ya ujenzi wa Madarasa ambayo yatamaliza uhaba wa madarasa na kuondoa mrundikano wa wanafunzi darasani.

Pia Mkuu wa Wilaya amemwagiza Mkurugenzi kuhakikisha shule zote shikizi za Msingi zinasajiliwa haraka ili shule zitakapofunguliwa wanafunzi wa darasa la kwanza waanze kusoma kwenye shule hizo.

Kwakumalizia Mhe. Mchembe ametoa maagizo kuwa shule zitakapofunguliwa wanafunzi wote waliofaulu wanatakiwa kwenda kuripoti kwenye shule zao walizopangiwa  na kama kuna wazazi wamewapeleka watoto zao kufanya kazi za ndani watawakamata wazazi na katoa maagizo kuwa watendaji na wenyeviti wote wafuatilie wanafunzi wanotakiwa kwenda shuleni waende shule.

Akisoma taarifa ya Halmashauri Mkurugenzi Mtendaji Bw. Saitoti Zelothe Stephen amesema wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wanampongeza Rais wa awanu ya sita  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta jumla ya kiasi cha Shilingi  bilioni mbili na milioni miambili za UVIKO-19 kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya vyumba vya madarasa 72 kwa shule za Sekondari na shule shikizi 7 za Msingi pamoja na miundombinu ya afya ya jengo la Huduma za dharura na nyumba ya mtumishi wa Afya. Amesema utekelezaji wa miradi hii ulitumia njia ya (FORCE ACCOUNT)  na kuweza kuokoa kiasi cha shilingi 89,024,420.50

Bw. Saitoti alisema ujenzi huu umemaliza uhaba wa vyumba vya madarasa  ambao wangepata wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza na darasa la kwanza kwa mwaka 2022, ambapo amesema kwa mwaka 2022 wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ni 5,717 kati yao wasichana 3,024 na wavulana 2,693. Aidha amesema kati ya shule shikizi 7 zilizoletewa fedha za UVIKO19 shule 4 zinafanyiwa utaratibu wa kupata usajili ili kuwapunguzia wanafunzi adha ya kutembea umbali mrefu, shule hizo ni Kwemigunga, Kwachiti, Tengwe na Kwambalu.

Alihitimisha kwa kusema kuwa fedha za miradi hiyo imesaidia pia kukuza uchumi wa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwa kupata ajira za muda za ujenzi kwani waliweza   kuajiriwa watu 819 lakini pia mama ntilie waliokuwa wanauza vyakula na vinywaji kwa wafanayakazi waliweza kujipatia kipato.

MWISHO.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Siriel Mchembe, akitoa maelekezo ya Wilaya  kuhusu majengo ya madarasa yatokanayo na fedha za UVIKO-19

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Saitoti Zelothe Stephen akisoma  taarifa ya madarasa ya UVIKO-19 mbele ya mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wiliaya ya Handeni.

Wakuu wa Idara na vitengo wa Halmashauri ya Handeni wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya wakati wa makabidhiano ya Madarasa ya UVIKO-19.

Wananchi mbalimbali waliojitokeza kwenye makabidhiano ya madarasa ya UVIKO-19.

Madarasa ya Shule ya Sekondari ya Martine Shigele yaliyojengwa kwa fedha za UVIKO-19.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa