• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

UONGOZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI UMEKABIDHI MATREKTA 4 KWA VIKUNDI VINNE NA KUVITAKA VIKUNDI HIVYO KUCHOCHEA KASI YA MAENDELEO YA KILIMO KWA KUTUMIA ZANA BORA.

Imerushwa: November 2nd, 2017

Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  umekabidhi matrekta manne (4) kwa vikundi vya uzalishaji na kuvitaka vikundi hivyo kutumia matrekta hayo kwa lengo la kuchochea kasi ya maendeleo ya kilimo kwenye maeneo yao.

 Akikabidhi  matrekta hayo Mwenyekiti  wa  Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Ramadhani Diliwa amewaeleza vikundi kuwa Halmashauri imeamua kuwapa matrekta hayo kama mtaji kutokana na utayari wa vikundi vyenyewe kwani vikundi vipo vingi ambavyo vingeweza kupewa na hivyo watambue wanao wajibu wa kuyatunza  na yasiwe chanzo cha migogoro.


 Amesema kuwa Halmashauri inatekeleza ilani ya chama cha mapinduzi ya kuhudumia wananchi, matrekta yaliyotolewa wangeweza kutoa hata kwa mtu mmoja mmoja lakini yametolewa kwa vikundi ili kuchochea maendeleo na kurahisisha utunzaji wa mradi huo.

 “kasaidianeni matrekta haya yakachochee na kuboresha kilimo, kuongeza uzalishaji na tija asitokee mtu mmoja kati yenu akawa ni chanzo cha mafarakano, Halmashauri haitavumilia tutawapokonya na kuwapa wahitaji wengine” alisema

 Ameongeza kuwa  matrekta yote matengenezo yake yapo chini ya Suma JKT hivyo iwapo kutatokea hitilafu yoyote wasitumie mafundi  wa mitaani kuyatengeneza badala yake yafikishwe kwa walengwa wa matengenezo, na kuwataka wasitumie mradi huo kwa lengo la kujinufaisha mtu binafsi.

 Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni William Makufwe amesema kuwa  matrekta yamekabidhiwa kwa vikundi kwa kuamini vitarahisisha katika  utunzaji  na kuvitaka vikundi hivyo kutumia matrekta hayo kama iivyokusudiwa kwa kuzingatia muda wa kufanya kazi na kuyapumzisha ili yaweze kudumu.

 Aidha ameongeza kuwa matrekta yote mbali ya kuwa mali ya vikundi lakini yapo kwenye Vijiji hivyo ni wajibu wao kutoa taarifa ya  usimamizi wa matrekta hayo kwenye uongozi wa Vijiji  ikiwa ni pamoja na kuwasilisha  mapato ghafi (10%ya mapato) kwenye miradi ya maendeleo ya Vijiji vyao  na mwisho wa siku kuongeza uzalishaji utakaopelekea  wananchi kuishi kwa amani na utulivu.

 “Matrekta haya ni mradi kama ilivyo miradi mingine , naomba yasiwe chanzo cha migogoro,kuwepo na uaminifu na uwazi katika kuendesha mradi, hii ni mali ya kikundi sio ya mtu binafsi na taarifa zote ziwekwe kwenye maandishi ikiwa ni pamoja na kuziwasilisha  kila baada ya miezi mitatu.” Alisema Mkurugenzi.

 Halmashauri iliingia makubaliano na vikundi vya wakulima kuchangia 20% kwa aajili ya matengenezo  ya matrekta  ambapo Halmashauri imetumia zaidi ya Tsh.36,218,000/= kwa ajili ya kununua vipuri mbalimbali katika kuyakarabati matrekta  kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya zana bora za kilimo.

 Vikundi vilivyokabidhiwa leo matrekta  ni pamoja na Kikundi cha Amani Vicoba Misima, umoja wa marafiki Mkata, kikundi cha wakulima Mandera na  kikundi cha maziwa Kwamsisi Saccos. Vikundi vyote vimeshukuru kupokea Matrekta hayo na kuahidi kuyatunza vizuri.


Image may contain: 8 people, people smiling, people standing and outdoor

Mwenyekiti wa Halmashauri Mh Ramadhani Diliwa akikabidhi mkata kwa moja ya kikundi cha wakulima.

Image may contain: 2 people, people standing, tree and outdoor

Mkurugenzi Mtendaji mwenye shati nyeupe akipata maelezo machache kutoka kwa mwendeshaji wa trekta aliyeshika usukani.

Image may contain: 1 person, sky, tree and outdoor

Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Ramadhani Diliwa akifanya majaribio kwenye moja ya Trekta kabla ya kukabidhi kwa wanavikundi.

  Image may contain: 2 people, people standing, sky and outdoor

Menyekiti wa Halmashauri Mh.Ramadhani Diliwa akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji William Makufwe wakizungumza wanavikundi.

Image may contain: sky and outdoor

Baadhi ya Matrekta yaliyotolewa na Uongozi wa Halmashauri.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa