• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO IMEFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI NA KUPONGEZA JENGO LA UPASUAJI MKATA.

Imerushwa: August 16th, 2017

Kamati ya Fedha Uchumi na Mipango(FUM) kwa kuambatana na wataalamu mbalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wamefanya ziara ya ukaguzi wa miaradi ya maendeleo kwa lengo la kujua hali halisi ya miradi , mahali ilipofikia na thamani ya pesa iliyotumika ( value for money).

Maeneo yaliyotembelewa na Kamati ya FUM ni pamoja na mgodi wa madini wa magambazi, maabara ya shule ya Sekondari Kwaluguru,jingo la upasuaji lililopo kwenye kituo cha afya cha Mkata na ujenzi wa bweni la wavulana shule ya sekondari Kisaza.

Katika ziara hiyo Waheshimiwa madiwani wamefanikiwa kupata maelezo ya lini mgodi wa magambazi utaanza kufanya kazi rasmi na namna ambavyo  wameshirikisha  jamii na wataendelea kushirikisha jamii kwa  kutoa ajira zinazoweza kufanywa na wazawa wa eneo hilo,kushiriki katika shughuli za kijamii zinazowagusa moja kwa moja wananchi na utoaji wa kodi kwa Serikali kuu na Halmashauri.

Kamati imeagiza pia miradi ambayo imechukua muda mrefu kukamilika, iweze kukamilika kwa wakati ili wanufaika wa miradi hiyo waweze kupata huduma bora kwa wakati unaostahili.

Aidha Kamati imepongeza ujenzi wa jengo la upasuaji lililopo katika kituo  cha afya cha Mkata kwa namna ambavyo thamamni ya fedha imeonekana wazi katika ujenzi wa jengo hilo na uwepo wa baadhi ya vifaa vinavyohitajika.

Kwenye miradi ambayo wananchi wanapaswa kushiriki  nguvu kazi Kamati imeagiza viongozi wa Kata na maeneo husika kuhakikisha wanahamasisha wananchi kujitokeza kushiriki nguvu kazi ambazo wanazoweza kufanya ili  kusaidia ukamilishwaji wa miradi kwa wakati, hasa ukizingatia miradi hiyo ni kwaajili ya manufaa yao na jamii nzima inayozunguka eneo husika hivyo, wanaowajibu kuhakikisha wanashiriki kikamilifu na kuumiliki mradi uliopo kwenye maeneo yao  ili  uweze kutunzwa vyema na wananchi wenyewe.

Kamati ikipata maelezo mafupi namna mtambo unavyochakata mchanga hadi upatikanaji wa dhahabu Magambaz.

Mtambo wa kuchakata mchanga hadi hatua ya kupatikana dhahabu.

Eneo ambalo CANACO Wataendelea kuchimba kuelekea mlimani ili kupata dhahabu.

Kamati ikipata maelezo kutoka kwa msemaji wa CANACO juu ya matumizi ya mitambo inayotumika kulainisha mawe ili wapate dhahabu.
Kamati ikipata maelezo mafupi juu ya jengo hilo.


Kamati ikitoka kwenye jengo la upasuaji kituo cha afya Mkata.


Kamati ya FUM na wataalamu mbalimbali wakiwa kwenye jengo la bweni la wavulana shule ya sekondari Kisaza.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa