• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Handeni yafanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo

Imerushwa: May 7th, 2020

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Handeni yafanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kuangalia utekelezaji wa ilani ya Chama tawala.

Kamati hiyo iliyoongozwa na mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Handeni Mh.  Athumani Malunda ilifanya ukaguzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni linaloendelea kujengwa. Pia  kamati  hiyo ilikagua kiwanda cha kuchakata mihogo cha kina mama Jipemoyo klilichopo kata ya kitumbi.

Mwenyekiti aliwashukuru wajumbe wa kamati ya siasa kwa kufanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya Halmashauri ya Handeni.

Pia aliwapongeza Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni pamoja na wafanyakazi wa Halmashauri kwa kuitekeleza vizuri ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo. Mwenyekiti huyo aliwakumbusha wajumbe Kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa hatari wa Korona (COVID 19).

Mh. Athumani  Malunda katika kiwanda cha kuchakata mihogo cha kina mama jipemoyo kilichopo kata ya kitumbi  alisema kuwa kumwezesha mwanamke sio kumpa pesa bali kumwanzishia mradi ndiyo utakaomwezesha kupata pesa ambazo ni endelevu.

Kwaupande wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe alimshukuru Mkurugenzi na wafanayakazi kwa ushirikiano  wao katika utekelezaji wa miradi mbalimbali na kuweza kuifanya Handeni iwe na ongezeko la kimaendeleo.

Mkuu wa Wilaya alimuagiza Meneja wa wakala wa barabara mjini na vijijini (TARURA) Wilaya ya Handeni  kurekebisha barabara inayoanzia kwenye barabara  kuu (Chalinze-Segera) inayoelekea kwenye jengo la makao makuu ya ya Halamshauri. Mh Godwin  Gondwe  amemuagiza meneja wa TANESCO Wilaya ya Handeni  kuhakikisha anaweka nyaya za umeme kwenye nguzo zilizisimikwa kuelekea  kwenye eneo la ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halamshauri ya Handeni. 

Katibu tawala wa Wilaya ya Handeni Mh. Mwl Boniphace Maiga amewaelekeza Maafisa  elimu wa Halmashauri  kuandaa vitini vya maswali hasa kwa madarasa ya mitihani na kufanya mawasiliano na wazazi wa wanafunzi hao kuja kuchukua na kuwapelekea watoto wao wakayafanye maswali hayo na kuyarudisha kwa walimu kwaajili ya tathimini ya upimaji wa maendeleo yao.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  Bw.William Makufwe aliishukuru kamati hiyo kwa kufanya ziara ili kupima utekelezaji wa miradi katika Halmashauri yake. Pia Bw. Makufwe alisema mradi wa ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri linaendelea vizuri mpaka sasa limefikia 20% na kueleza changamoto zinazozikabili ujenzi wa jengo hilo kuwa ni mvua na ubovu wa barabara inayopelekea vifaa vya ujenzi kushushwa eneo lingine na kuchukua usafiri mwingine na kuongezeka kwa gharama za ziada.  Mkurugenzi  Mtendaji amesema kuwa pesa za kuwawezesha  kiwanda cha kuchakata mihogo cha kina mama Jipemoyo kilichopo kata ya Kitumbi  zimetokana na mapanto ya ndani ya Halmashauri. Aidha Mkurugenzi amesema tayari kunamazungumzo yanaendelea kuhusu makubaliano na kampuni kutoka Dar es salaa itaingia mkataba na kiwanda hiko na kununua unga wa muhogo tani mia moja (100).

Kwapamoja wajumbe wa kamati ya siasa ya Wilaya ya Handeni  wamemuelekeza Meneja wa TANESCO kupeleka umeme kwenye kiwanda cha kuchakata mihogo cha kina mama jipe moyo kilichopo kata ya kitumbi kwaajili ya kuongeza uzalishaji kiwandani hapo.

Mwenyekiti wa kamati ya siasa ya Wilaya ya Handeni Mh. Athumani Malunda aliyeshika karatasi akitoa ufafanuzi kwenye ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri ya Handeni.

Mh. Athumani Malunda wa kwanza aliyetangulia akiwa na wajumbe wa kamari ya siasa ya Wilaya wakikagua barabara inayoelekea kwenye jengo la makao makuu ya Halmashauri ya Handeni.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni aliyetangulia mbele akitoa maelekezo ya ujenzi wa barabara inayoelekea kwenye jengo la makoa makuu ya Halmashauri ya Handeni.

Katibu tawala wa Wilaya ya Handeni Mh. Mwl Boniphace Maiga akifafanua jambo kwenye ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri ya Handeni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe akitoa ufafanuzi wa ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri ya Handeni.

Kamati ya siasa ya ya Chama cha Mapinduzi ya Wilaya ya Handeni ikiwa kwenye kiwanda cha kuchakata mihogo cha kina mama jipemoyo kilichopo kata ya kitumbi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa