• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Katibu tawala afungua siku ya mkulima Handeni

Imerushwa: September 24th, 2020

Katibu tawala wilaya ya Handeni Mhe. Mashaka Boniphace Mgeta amefungua maadhimisho ya siku ya mkulima Handeni yaliyofanyika kwenye kijji cha Suwa kata ya Mazingara.

Mhe. Mgeta amemshukuru mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri na wafanyakazi wote wa Handeni kwa ushirikiano na kufanikisha siku ya mkulima pia  amewapongeza wadau wa kilimo cha muhogo na taasisi zote za utafiti kwa juhudi kubwa za kuhakikisha wakulima wa muhogo wanalima kwa kutumia mbegu bora ili kupata mazao yenye tija kwaajili ya chakula na kujiongezea kipato na amewaagiza maafisa ugani wote kuwatembelea wakulima shambani ili kutoa ushauri wa kitaalam kwa wakulima.

Kwakuhitimisha  Mhe. Mashaka Mgeta amewahasa wazazi kutumia kilimo chenye manufaa ili kuwasomesha watoto wao hususani wa kike na mzazi ambaye mtoto wake hajampeleka shule sheria za mtoto zipo na zitachukuwa mkondo wake na mapango wa elimu Handeni kila Tarafa kuwe na kidato cha tano na sita hivyo wazazi wapeleke watoto wao shule.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. William Makufwe amemshukuru Katibu tawala wa wilaya ya Handeni pamoja na wanachi waliojitokeza kushiriki kilele cha siku ya Mkulima Handeni.

Bw. Makufwe amesema kuwa ameanza kuhamasisha zao la muhogo wilaya ya Handeni tangu mwaka 2016 kutokana na njaa kwenye wilaya ya Handeni hivyo kwa kushirikiana na wataam wa Halmashauri wameondoa janga la njaa kwa kuhimiza kila familiya kulima heka tatu za muhogo kwa kufuata mashariti ya kilimo cha muhogo kuzingatia ushauri wa wataalam waliopo kwenye kila kata.

Kwakumalizia Bw. Makufwe amesema kuwa wawekezaji kutoka Dubai wanajenga kiwanda cha kuchakata muhogo kwenye Halmashauri ya Handeni na watahitaji tani 300 za muhogo  kila siku kwaajili ya kiwanda hicho hivyo mahitaji ya muhogo ni makubwa ndani ya Handeni na nje kwani kila siku magari yanapekeka kuuza  muhogo kwenye masoko ya Dar es Salaam.

Katibu tawala wilaya ya Handeni Mhe. Mashaka Mgeta, kulia aliyevaa koti akimsikiliza afisa kilimo wa Halmashauri ya Handeni aliyeshika karatasi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe wapili kushoto akisikiliza maelezo kuhusu ubora wa mbegu ya muhogo aina ya Pwani kutoka kwa mtafiti wa mazoa ya mizizi Dkt. Esther Masumba.

Afisa kilimo wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. Yibarila K. Chiza aliyesimama akiongea jambo kwenye maadhimisho hayo.

Dkt. Esther Masumba mtafiti wa mazao ya mzizi akielezea aina ya magonjwa yanayoshambulia zao la muhogo. 

Mbegu ya Muhogo aina ya Pwani hutoa mazao zaidi ya tani hamsini (tani 50) kwa hekari moja.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa