• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Katibu tawala wa mkoa wa Tanga afanya ziara ya kukagua miradi ya elimu Handeni Vijijini

Imerushwa: May 15th, 2020

Katibu tawala wa Mkoa wa Tanga Bi. Junica Omari amefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo ya sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na madarasa yaliyojengwa kwa fedha za  Lipa kulingana na matokeo (EP4R) katika Halmashauri ya Handeni.

Bi. Junica Omari amekagua majengo ya madarasa katika shule za Kabuku sekondari, Shule ya msingi Kabuku nje, Shule ya msingi Kwedikwazu Mashariki, Shule ya sekondari Kisaza,Shule ya sekondari Kitumbi na Shule ya msingi Mhalango. Katibu tawala Mkoa wa Tanga Bi.Junica Omari amewapongeza walimu, watumishi wa Halmashauri, wazazi, wanafunzi na wadau wa elimu kwa jitihada za kuingeza ufaulu wa darasa la saba na kidato cha nne mwaka 2019.

Amesema matokeo mazuri yanaonesha kuwa Handeni wamejipanga kwa kufanya vizuri kwenye sekta ya elimu na amewakumbusha watumishi kuwa na mahusiano mazuri wawapo kazini kwakuwa maendeleo yanapatikana kwa ushirikaiano wa wafanyakazi wote

Bi. Junica Omari amewaasa watumishi kufanya kazi na kuacha kutafuta visingizio vya kuhama pale walipo sasa na ameongeza kuwa watumishi lazima wawe wabunifu wawpo kazini ili kutoa ufanisi mzuri na matokeo makubwa.

 Afisa elimu mkoa wa Tanga Bi. Mayasa Hashim amemuambia katibu tawala mkoa wa Tanga kuwa uongozi wa Halamshauri ya Handeni pamoja na wafanayakazi wanafanya kazi kwa ushirikiano na wanatekeleza kwa wakati kila jukumu wanalopewa.

Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe amemueleza katibu tawala wa mkoa wa Tanga kuwa kwa sasa shule zote za Halmashauri ya Handeni zinapata chakula cha mchana kwakuwa  kila shule inalima mihogo hekari tatu, mahindi hekari tatu kwaajili ya chakula na korosho hekari tatu kwaajili ya biashara.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe  amemshukuru Katibu tawala wa mkoa kwa kufanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri yake na kumuahidi kuwa yeye pamoja na wafanyakazi wote wa Halmashauri watasimamia kikamilifu miradi yote iliyopo kwenye Halmashauri hiyo. 

MWISHO.

Katibu tawala mkoa wa Tanga Bi. Judica Omari kushoto akisalimiana na watumishi wa Halmashauri ya Handeni.

 Bi. Judica Omari akinawa mikono kujikinga na korona alipowasili ofisi za Halmashauri ya Handeni.

 Katibu tawala mkoa wa Tanga Bi.Judica Omari akikagua ofisi za muda za  halamsahauri ya Wilaya ya Handeni. 

Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Gondwin Gondwe mbele akimuongoza katibu tawala mkoa wa Tanga kukagua ofisi za muda za Halmashauri ya Handeni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe mwenye koti jeusi akitoa ufafanuzi mbele ya katibu tawala mkoa wa Tanga Bi.Judica Omari alipotembelea ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Handeni.

Watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni wakimsikiliza Katibu tawala mkoa wa Tanga.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa