• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maadhimisho ya MEIMOSI yafana Handeni

Imerushwa: May 2nd, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imeungana na wafanyakazi wote duniani kuadhimisha siku ya wafanyakazi ambayo hufanyika kila mwaka ifikapo tarehe 01-05, Kwa mwaka huu siku hiyo imebeba kauli mbiu inayosema “Uunganishaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii ulenge kuboresha mafao ya mfanyakazi”, kilele cha maadhimisho hayo yalifanyika jana  katika viwanja vya Chanika ambapo mgeni rasmi  alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe.

Katika maadhimisho hayo Katibu wa vyama vya wafanyakazi Ndugu Hamisi Ngomero  amesema tunapenda kuikumbusha serikali kupitia maadhimisho haya kuendelea kuboresha maslahi ya watumishi sambamba na  maboresho yanayoendelea kufanyika serikalini na katika mifuko ya hifadhi ya jamii na kwamba suala la uhakiki limeshakamilika tangu septemba 2017 hivyo serikali ifungue upandishwaji wa madaraja kwa watumishi wake.

Ameongeza kuwa watumishi wa Handeni wanakumbana na kero ambazo zinarudisha nyuma ari ya utendaji kazi,  kero hizo ni madai mbalimbali ya watumishi yaliyokwisha hakikiwa hayajalipwa kama malipo ya uhamisho, masomo, matibabu, kustaafu, likizo, posho ya kujikimu, fedha za kujikimu ajira mpya na stahiki za viongozi na kulazimisha wafanyakazi kulipishwa michango mbalimbali bila hiari yao.

Aidha  aliwashukuru waajiri kwa kudumisha mahusiano mazuri baina wafanyakazi, vyama vya wafanyakazi  na waajiri, kulipa kwa sehemu madeni ya watumishi, waaijiri kulipa mishahara ya watumishi wao kwa wakati, kuondoa watumishi hewa, kuhimiza mifuko ya hifadhi ya jamii kulipa mafao ya watumishi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe ambaye pia ni mgeni rasmi amesema serikali ya awamu ya tano imehakikisha kuwa wafanyakazi hewa wanaondolewa kwani  bila kuondoa wafanayakazi hewa kwanza maana yake watapandishwa vyeo kwa hiyo serikali imeona ni vyema kuhakiki vyeti kabla ya kupandisha madaraja na kwamba serikali imeanza kupandisha madaraja tangu Novemba  2017 baada ya uhakiki huo kukamilika ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwa mwaka 2017/2018 itapandisha madaraja wafanyakazi elfu moja mia mbili ishiri na nne (1224),  kwa upande wa madeni serikali ilisitisha kulipa ili isiwe inalipa madeni hewa pia ambayo itakuwa hasara kwa serikali kulipa madeni ya watumishi hewa kwa hiyo kwa vile uhakiki umeshakamilika madeni ya watumishi yatalipwa.

Amewataka waajiri kushirikisha kwanza vyama huru vya wafanyakzi kabla ya kuwatoza watumishi michango ya aina yoyote katika ngazi yoyote ile na wafanyakzi waelimishwe kwanza na wao kwa hiari yao ndiyo watatoa hiyo michango na pia amewataka maafisa utumishi kuhakikisha wanasimamia makato ya watumishi yanaenda kwenye mifuko ya hifadhi ya kijamii  kwa sababu ni haki yao ya msingi na kuahidi kulisimamia hilo ”nawaahidi nitalisimamia itavyotakiwa” alisema.

Pia aliwapongeza wafanyakazi wote kufanyakazi kwa moyo pamoja na changamoto wanazokutana nazo na amewapongeza waliochaguliwa kuwa wafanyakazi bora kama wawakilishi wa wafanyakazi wote ”lakini nyinyi ni wawakilishi wa wafanyakazi wote maana hamuwezi kuwa wafanyakazi bora wote kwa wakati moja” amesema.

Amehitimisha kwa kuwataka wananchi wote kuwa wavumilivu kutokana na  tatizo la mda mrefu la maji  Handeni  kwani limepata ufumbuzi, amesema waheshimiwa Mbunge wanalifanyia kazi na baada ya wiki mbili tutakuja kutangaza tena kwa wananchi akiwepo na mkandarasi na kwamba makubaliano yatafanyika mbele ya wananchi ili mkandarasi huyo akianza kazi amalize  kwa wakati unaotakiwa na pia kazi ifanyike kutokana na thamani ya fedha iliyotolewa  amesema ”hilo tunalifanyia kazi pamoja na wabunge na viongozi wote”

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa