• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MADIWANI NA WATENDAJI WA KATA WASHAURIWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO INAYOFADHILIWA NA MASHIRIKA YASIYO YA SERIKALI ILI KULETA TIJA

Imerushwa: October 16th, 2017

Madiwani na Watendaji wa kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni mkoani Tanga,wameshauriwa kuhakikisha wanasimamia vizuri miradi ya maendeleo hususani inayofadhiliwa  na mashirika yasiyo ya kiserikali iliyopo kwenye maeneo yao ili iweze kujengwa kwa kiwango kinachohitajika.

 Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hamlamashuri ya wilaya ya Handeni William Makufwe kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika Oktoba 16 na kueleza kuwa kuna umuhimu wa viongozi wa Kata kuwa karibu na wafadhili wanaojenga miradi kwenye maeneo yao kwani wao ndio wasimamizi.


 Makufwe alisema ofisi ya Mkurugenzi inakuwa na imani kwamba Madiwani na Watendaji wa Kata ndio wasimamizi wakuu wa miradi iliyopo kwenye kata zao hivyo ikitokea miradi haina kiwango ina maana viongozi ngazi ya Kata hawakutimiza wajibu wao.

 Aliongeza Kuwa ni kweli Serikali inahitaji kufadhiliwa lakini sio kwa kujengewa miradi ambayo ipo chini ya kiwango hali inayopelekea  kuharibika Kwa muda mfupi na kutokufikia malengo yaliyokusudiwa.

 " Waheshimiwa mnaopata miradi hii ya ufadhili hakikisheni inaleta tija kwa kusimamia hususani wanaopewa tenda ya kujenga kuepuka madhara yanayoweza kuepukika kwa kuisimamia tu" alisema Makufwe. 

 Kwaupande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni,Ramadhan Diliwa alisema kuwa kuna baadhi ya miradi ni kweli mapungufu yapo na yamesababishwa na kutokuwepo uangalizi wa karibu na kusisitiza Madiwani kusimamia vyema miradi kwa manufaa ya wananchi wao. 

 Alitolea mfano eneo la Kata ya Kabuku mjini kuwa kuna madarasa yaliojengwa na wafadhili miaka iliyopita lakini ipo chini ya kiwango hali iliyopelekea wanafunzi kutolewa ndani ya madarasa hayo na kutafutiwa mengine kutokana na kuwa hatarishi kwao.

 Aidha Sharifa Abebe diwani kata ya Kwamgwe alisema ni kweli awali hali kama hiyo ilikuwa ikitokea ila kwasasa wanasimamia vizuri miradi iliyopo kwenye maeneo yao ambapo kwake ipo miradi inayofadhiliwa na inajegwa katika ubora unaohitajika kutokana na usimamizi uliopo Kwa kushirikiana na watendaji ngazi ya Kata.


Image may contain: 2 people, people sitting

Meza kuu

Image may contain: 2 people, people sitting

Diwani wa Kata ya Kwamgwe Mh.Sharifa Abebe akizungumza na wataalamu na madiwani kwenye kikao cha baraza. 

  Image may contain: 1 person, standing and hat

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni William Makufwe akitioa ushauri kwenye kikao cha Baraza.

Image may contain: one or more people, people sitting and indoor 

wataalamu na Madiwani wakiwa kwenye kikao cha baraza ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya.






Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa