• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mradi wa kuongeza mnyororo wa thamani wa mazao ya misitu watambulishwa Handeni

Imerushwa: May 19th, 2019


Elimu ya kulinda mazao ya misitu imefanyika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kupitia programu ya kuendeleza mnyororo wa thamani wa mazao ya misitu (FORVAC) iliyoendendeshwa na Idara ya Misitu na maliasili ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

Utambulisho huo wa mradi ulifanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni mwishoni mwa wiki iliyopita kwa Kamati ya ulinzi na usalama, waheshimiwa madiwani, wakuu wa Idara, Maafisa Tarafa na Watendaji Kata.

Akitoa maelezo ya mradi, Mratibu wa progaramu Bw. Petro Masolwa alisema lengo la mradi ni kuongeza faida za kiuchumi, kijamii na kimazingira kutokana na usimamizi endelevu wa rasilimali za misitu pamoja na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi kwenye sekta ya misitu.

Amesema programu imefanywa kwa ufadhili wa serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na serikali ya Finland ambapo kwa Tanzania mikoa iliyopata ufadhili huo ni Lindi, Tanga, Dodoma na Ruvuma na kwa Mkoa wa Tanga utanufaisha Wilaya ya Handeni katika maeneo ya Mazingara, Kwedikabu, Kwamsundi, Kitumbi na Gole na Wilaya ya Kilindi.

Aidha, amesema programu itawajengea uwezo serikali za vijiji na kamati za maliasili, Halmashauri, Wizara na wadau mbalimbali kwenye usimamizi shirikishi wa rasilimali za misitu pia progrmu itwezesha kuingizwa kwa mafunzo/elimu ya uendelezaji wa mnyororo wa thamani wa mazao ya misitu na masoko katika mitaala ya vyuo husika.

Pia amesema programu itawezesha uboreshaji wa huduma za ugani na mawasiliano katika sekta ya misitu na kuanzisha ufuatiliaji na usimamizi wa taarifa sambamba na uboreshaji wa sera na sheria za misitu, utawala na biashara ya mazao mbao zilizovunwa kwenye misitu iliyohalalishwa kuvunwa.

Alihitimisha kwa kuwataka wadau kusimamia misitu hiyo ili kuleta matokeo chanya yatakayoendeleza ufadhili kwasababu Wilaya ambazo zitafanya vizuri ndizo zitakazoongezewa ufadhili na zile ambazo zitafanya vibaya hazitaletewa ufadhili huo hata kama zilikuwepo kwenye programu.

Kwa upande wake Afisa misitu Bw. Elinihaki Mdee akijibu maswali ya wadau kuhusu uharibifu wa misitu na mipaka ya kazi kati ya misitu inayosimamiwa na vijiji na misitu inayosimamiwa na Wakala wa misitu alisema maafisa misitu wa Halmashauri na Wakala wa misitu wanashirikiana kusimamia misitu yote iliyoko ndani ya Wilaya tofauti ni katika mipaka ya kiutawala kuwa msitu fulani ni wa serikali kuu na mwingine ni wa Halmashauri au wa kijiji. Kwa upande wa uharibifu wa misitu alisema hakuna namna yoyote yakuvuna msitu bila mpango wa uvunaji wa rasilimali ya misitu iliyopo hivyo uvunaji unafanyika kulingana na kiasi kitakachostahili kuvunwa kwa mwaka na mtu akifanya zaidi ya kiasi hicho basi ni kiume cha sheria.

Bw. Mdee alitoa wito kwa wadau kushirikiana katika kusimamia misitu bila kutegemea maafisa misitu pekee kwasababu wananchi ndiyo ambao wapo katika maeneo ya misitu hivyo taarifa zitolewe pale ambapo kuna uharibifu au uvamizi ili kuchukua hatua kwa wakati.

MWISHO.

Mratibu wa programu Bw. Petro Masolwa akitoa mafunzo.

Afisa misitu Bw.Elinihaki Mdee akijibu maswali ya wadau


Wadau wakifuatilia mafunzo.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa