• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mafunzo ya wawezeshaji wa Mpango wa (TASAF) awamu ya tatu yafunguliwa Handeni DC

Imerushwa: April 10th, 2018


Wawezeshaji wa Mpango wa (TASAF) wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni watafanyiwa mafunzo ya siku tano  ambapo watafanyiwa mafunzo ya nadharia na vitendo kuhusu utaratibu wa uundaji wa vikundi vya kuweka akiba kwa walengwa wa mpango wa kunusuru Kaya maskini awamu ya tatu.

Mafunzo hayo yalifunguliwa jana tarehe 09-04-2018 na Mgeni rasmi Bw.Willam Makufwe ambaye pia ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni   katika ukumbi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC). Mgeni rasmi aliwashukuru viongozi wa TASAF Makao makuu kwa kuleta programu hiyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwani watanusuru Kaya maskini kutoka katika hali waliyonayo kwenda hatua nyingine kiuchumi kwa sababu jamii ikipata elimu ya kuweka akiba itajihusisha na ujasiriamali ikiwemo kilimo,ufugaji na biashara mbalimbali itakayowaingizia kipato.Pia aliwataka wawezeshaji wa kunusuru Kaya Maskini kutumia utaalamu wao ili kuhakikisha wanaelimisha jamii na mwisho wa siku zoezi linafanikiwa kwa kiwango kinachotakiwa.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa TASAF makao makuu ambaye pia ni Afisa Mawasiliano TASAF Makao makuu Bw. Estom Sanga Wakati wa ufunguzi huo aliwaeleza wawezeshwaji kuwa programu hii ya kukuza uchumi wa Kaya maskini inahusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali ambazo zitasaidia ukuaji wa uchumi wa Kaya. Shughuli hizo zinahusu uhamasishaji wa walengwa kuunda vikundi vya kuweka akiba  ambazo zitatumika na walengwa  kama mitaji ya kuanzisha au kupanua shughuli zao za kiuchumi.Aidha, walengwa wanatarajia kupata ujuzi utakaowasaidia kutekeleza miradi au biashara zao kwa faida na endelevu hivyo kuongeza kipato chao na pia kupunguza umaskini.

Aliongeza kuwa uanzishaji wa program hii utalazimu kuwa na wawezeshaji wengi wenye ujuzi wa kuwaelezea walengwa jinsi shughuli za program hii zitakavyofanyika  katika nyakati tofauti na utaratibu wa uendeshaji wa mafunzo utakuwa jumuishi ili kuwezesha walengwa kuwa na shughuli zenye tija hivyo njia ya ushirikishaji zitatumika katika ngazi ya  jamii kwani lengo ni kuiwezesha Kaya kumudu mahitaji yake na kupata ziada ili kujikwamua kiuchumi na hivyo kuwatoa walengwa kwenye umaskini.

Pia alisema  utekelezaji wa mpango wa kunusuru Kaya maskini  unaendelea vizuri kwani hadi sasa unafanyika katika Vijiji, Mitaa na Shehia 9809 kwenye maeneo 161 ya Mamlaka za utekelezaji ikihusisha Tanzania Bara na Visiwani(Unguja,Pemba na Zanzibar). Idadi ya Kaya maskini zilizotambuliwa ni 1,369,649 na Kaya zilizoandikishwa kwenye mpango na zinazolipwa ni 1,106,071 na utekelezaji wa miradi ya kutoa ajira za muda imeanza katika Halmasahuri 44 hivyo mafunzo haya ni sehemu ya mkakati endelevu wa kuondokana na umaskini kwa kuwezesha Kaya hizo hizo za walengwa kuweka akiba na kufanya shughuli za kiuchumi

Aidha,aliongeza kuwa utekelezaji wa programu ya kukuza uchumi wa Kaya ulishaanza kutekelezwa katika Mamlaka nane za maeneo ya utekelezaji ambazo ni Chamwino, Bagamoyo, Kibaha, Mtwara MC, Lindi MC,Unguja na Pemba na jumla ya vikundi 5182 vimeundwa na mafunzo ya awali ya vikundi hivyo yanaendelea, Walengwa wameonyesha ari kubwa ya kuanza kuweka akiba. Changamoto iliyopo ni jinsi ya kuvifuatilia vikundi na kuvipa taaluma ya uendelevu ambayo inatarajiwa kufanywa na ninyi wakufunzi na ndiyo sababu tunapenda wakufunzi watoke ngazi ya Kata ili kurahisisha ufuatiliaji kwani bila kufanya hivyo ukuaji wa vikundi utakuwa ni changamoto.

Kwa upande wa mratibu wa TASAF wa halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bi Amina Luhizo alisema kuwa program hii itasadia kuweka Kaya maskini kwenye uchumi wa kati kutokana na kuwa vikundi vikiundwa na vikaweka akiba vitapata fedha za ziada ambazo zitawasaidia kufanya shughuli mbalimbali za ujasiriamali zitakazowaongezea kipato.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa