• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Afanya ziara Handeni.

Imerushwa: September 25th, 2021

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mpinduzi ya Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla  pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu  ya Chama Cha Mapinduzi Taifa na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga  amefanya ziara Mkoa wa Tanga na kutembelea Miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa Amewashukuru Wanahandeni kwa mapokezi makubwa hasa  akinamama wamejitokeza kwa wingi sana.

Mhe. Hemed Suleiman Abdulla  amempongeza Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha  kiasi cha Milioni 250 kwaajili ya ujenzi wa kituo cha afya Sindeni na amewahasa viongozi  wa Handeni kuwa fedha hizo zitumike vizuri kwa mujibu  wa matumizi yaliyokusudiwa kama ilivyoelekezwa bila mapungufu yoyote  na  Mkoa wa Tanga ni Mkoa unaotekeleza vizuri  Ilani ya Chama Cha Mapinduzi hivyo kazi hii itasimamiwa vizuri na kukamilika kwa wakati ili  wananchi  wa Sindeni na  Handeni  kwaujumla wapate kituo cha afya na huduma pia.

Kwakumalizia Mhe.  Hemed Suleiman Abdulla  amewataka  wananchi kujitokeza kwenye Sensa  ya watu na makazi ya mwaka 2022 ili wahesabiwe na Serikali  iweze kupata idadi sahihi na kupanga mipango ya maendeleo pia amewakumbusha  wananchi kujitokeza kwenda kupata chanjo ya ugonjwa wa uviko 19  kwani maradhi hayo bado yapo na selikali imeleta chanjo bila gharama  yoyote.

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mpinduzi ya Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akipanda mti kwenye eneo la ujenzi wa kituo cha Afya Sindeni.

 Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe.  Adam Kigoma Malima amemshukuru Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mjumbe wa Kamati Kuu  ya Chama Cha Mapinduzi Taifa na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga kwa kufanya ziara kwenye eneo la ujenzi wa kituo cha Afya Sindeni na kushiriki ujenzi wa jengo hilo.

Mkuu wa Mkoa amesema  watausimamia na kufuatilia  ujenzi huo na kuhakikisha ndani ya miezi Mitatu jengo la  wagonjwa wa nje,  Maabara na kichomea taka vitakuwa vimekamilika.

Mhe. Malima amewaahidi wananchi wa Sindeni kuwa  baada ya miezi mitatu maji na umeme vitakuwa  vimefika kwenye kituo cha afya  Sindeni na wananchi watapata huduma hizo kituoni hapo.


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe.  Adam Kigoma Malima.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Handeni  Dkt.  Kanansia Michael  Shoo akisoma taarifa ya upatikanaji wa huduma ya afya Handeni mbele ya Makamu Wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mpinduzi ya Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla  pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu  ya Chama Cha Mapinduzi Taifa na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga  amesema tunatoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzani Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha kiasi cha Shilingi Milioni mia mbili na hamsini kwaajili ya ujenzi wa kituo cha afya Sindeni. Tunatambua haya ni matokeo ya juhudi kubwa za Rais wetu kupitia makusanyo ya Tozo za miamala ya simu na sisi Handeni ni wanufaika wa tozo hizo.

 Dkt. Kanansia ameongeza kusema kuwa kituo cha afya Sindeni  kinatarajia kuhudumia wakazi wapatao 68,754 na ujenzi wa kituo hiki kitasogeza huduma karibu na wananchi sawasawa na matakwa ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya  Mwaka 2020-2025 yenye lengo la kuimarisha na kuongeza vituo vya kutolea huduma za Afya nchi nzima.


Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Handeni  Dkt. Kanansia Michael  Shoo akisoma taarifa.

Baadhi ya Madiwani pamoja na wananchi wa Sindeni waliojitokeza kwenye ziara hiyo.

Wananchi waliojitokeza kwenye Ziara ya Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa