• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Makamu wa Rais afanya ziara Handeni.

Imerushwa: March 16th, 2021

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Handeni,.

Mama Samia Suluhu ameweka jiwe la msingi kwenye jengo la makao makuu ya Halamashauri ya  Handeni linaloendelea kujengwa eneo la  Mkata pia amefungua kiwanda cha kusaga  mahindi na cha kutengeneza juisi kilichopo Segera.

Akiweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa jengo la makao Makuu ya Halmashauri, Mama Samia Suluhu amewashukuru wanahandeni kwa kukirudisha madarakani Chama Cha Mapinduzi hivyo watakamilisha ahadi zote zilizopo kwenye ilani ya chama na kukamilisha miundombinu yote pamoja na jengo hilo na amewapongeza Halmashauri kwa usimamizi wa fedha zinoletwa kwaajili ya maendeleo ya Handeni.

Aidha Makamu wa Rais Mhe. Samia amewaasa Watanzania kushikamana na kufanaya kazi ili kujenga uchumi  kuhakikisha Tanzania inasonga mbele.

Uanzishwaji wa mji mdogo Kabuku Mama Samia amesema Serikali ya mkoa na Wilaya ianze mchakato kisha wapeleke taarifa kama imekidhi  vigezo Kabuku utakuwa mji mdogo.

Kwakuhitimisha Makamu wa Rais Mh. Samia Suluhu amesema changamoto zote zilizopo kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi na ahadi ambazo Rais ameahidi zitatekelezwa zote na kuwahakikishia wananchi wote wanapata maji safi na salama, huduma za afya bora na fursa ya kupata elimu bure.

Kwaupande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe akitoa taarifa ya ujenzi huo mbele ya Makamu wa Rais, ameishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kutoa fedha kwaajili ya ujenzi wa makao makuu ya Halmashauri ya Handeni  na mpaka sasa ujenzi umefikia 40%.

Bwana Makufwe amesema walipofanya mapitio ya gharama za ujenzi ili kumpa mkandarasi kujenga jengo gharama za ujenzi ilikuwa billion 7.8  baada ya kuamua kutumia “force account”  ujenzi utakamilika kwa bilioni 5.3 na kuokoa kiasi cha biliaoni 2.5 ambazo zitatumika kwenye maeneo mengine.

Aidha Mkurugenzi  Makufwe amesema kuwa Halmashauri inapokea fedha za ujenzi kwa awamu na mpaka sasa  imepokea kiasi cha Bilioni 2 kwakutumia “force account” Halmashauri imeokoa kiasi cha Millioni 500. Ameongeza kusema kuwa jengo hilo la makao makuu ya Halmashauri litakapokamilika litakuwa na ofisi  209,  kumbi mbili za mikutano zitakazochukuwa watu 200 kila ukumbi na idara zote zitakuwa pamoja ili kurahisiha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa kumalizia Bw. Makufwe amezitaja changamoto kwenye ujenzi wa jengo hilo amesema kuwa  ubovu wa barabara kutoka barabara kuu kwenda eneo la ujenzi ilisababisha gari zilizokuwa zinapeleka vifaa kushindwa kufika eneo la ujenzi na kushusha vifaa hivyo eneo lingine na kusababisha gharama za zaidi na mvua kubwa zilizonyesha mwanzoni mwa mwaka 2020 ilisababisha kazi ya ujenzi kuchelewa.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu akipanda mti kwenye kiwanda cha kusaga mahidi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wapili kulia aliyeshika kitabu Bw. William Makufwe akitoa taarifa ya ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri mbele ya Makamu wa Rais.

Mhandisi John Mshahara, aliyevaa kofia ngumu akitoa maelezo ya ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri mbele ya makamu wa Rais.

Wakuu wa Idara pamoja na wananchi waliojitokeza wakimsikiliza Makamu wa Rais.

Jengo la makao makuu ya Halmashauri linaloendelea kujengwa.

Muonekano wa barabara inayoelekea kwenye ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri kabla ya kufanyiwa matengenezo.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa