• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MASHINDANO YA UCHUMI CUP YAMEMALIZIKA WILAYANI HANDENI KWA KUZINDULIWA RASMI MSIMU WA KILIMO HUKU VIBAONI FC WAKITAMBA KWA USHINDI.

Imerushwa: February 12th, 2018

 Mashindano ya UCHUMI CUP Wilayani Handeni yamemalizika jana katika viwanja vya Kigoda na timu ya Vibaoni FC ikiibuka na ushindi wa magoli 3 kwa 0 dhidi ya Kurugenzi FC, mashindano yaliyoasisiwa na  Mkuu wa Wilaya ya Handeni   yenye kauli mbiu ya “Kipaji changu Mtaji wangu” 

 Akizungumza kwenye fainali hizo Mkuu wa  Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe  alisema kuwa mbali na kupeana taarifa mbali mbali za fursa zilizopo Handeni UCHUMI CUP imelenga kuinua vipaji na uchumi wa  vijana , na kuwapongeza washindi na timu zote zilizoshiriki mashindano hayo kuanzia ngazi ya Tarafa hadi kufikia kwenye fainali.

 Mh. Gondwe alisema kuwa msimu wa kilimo umezinduliwa rasmi kwenye fainali hizo  kwani vijana wamepata uelewa na kuwahamsisha kulima mazao mbalimbali kama vile mahindi, korosho, mihogo na katani huku akiwataka vijana kuwa na walau na ekari ya Muhogo hususani katika kipindi hiki ambapo zao la muhogo linastawi vizuri.

 “Ardhi ya Handeni inarutuba na mazao mengi yanastawi vizuri, vijana mtumie fursa hii kujikuza kiuchumi kwa kulima mazao mbalimbali , uzuri zao la muhogo linastawi sana”Alisema Mh. Gondwe 

 Aliongeza kuwa  Ilani ya Chama inatekelezwa kwani michezo ni moja ya Ilani hivyo Uchumi Cup inatekeleza fursa aliyotolewa  na Rais wa Jamuhuriu ya Muungano wa Tanzania Mh.John Pombe Magufuli kwa kusapoti viongozi wa Mkoa wa Tanga na kuahidi kufanyika kwa michezo kila mara muda utakapopatikana.

 Aidha amepongeza timu ya mpira wa miguu kupanda daraja na kuingia kucheza ligi kuu msimu ujao Coastal Union kwa kuwakilisha vyema Mkoa wa Tanga na kusema Uchumi Cup ipo tayari kuwasapoti na kuwapa nafasi ya kuwachangia katika shughuli mbalimbali  ikiwemo kambi pindi itakapohitajika.

 Alisema kuwa vipaji vya mpira wa pete na miguu vimeonekana na vijana wameonesha uwezo wao, sasa imetengenezwa timu itakayokuwa inawakilisha Wilaya ya Handeni na itatafutiwa timu zilizoingia  ligi kuu ya Tanzania zije kucheza na Handeni kwa lengo la kupata msingi mzuri utakaowezesha timu ya Handeni kusonga mbele.

 Katika Mashindano ya Uchumi Cup mshindi wa kwanza Vibaoni Fc ametoka na zawadi za Jezi seti moja,TSh.300,000/=, kikombe cha dhahabu , mipira 3 na medali huku wafungaji wakiwa ni Hassani Ngilo aliyefunga magoli 2 na Shabani Mswagala bao 1. Mshindi wa Pili Kurugenzi FC amepata mipira 2, seti ya jezi na Tsh.200,000/=, huku mshindi wa tatu Mtazamo FC  akitoka na kitita cha Tsh.100,000/=, medali za shaba na jezi. Na mshindi wa nne aliyepata mpira 1 ametoka Umoja FC kutoka Segera huku washindi wote ngazi ya Tarafa wakipewa zawadi ya jezi seti 1.

 Kwaupande wa mpira wa pete mshindi wa kwanza ni Wanawake live waliowatoa kivesa Sekondari kwa bao 44 kwa 14, wamepata zawadi ya medali, jezi,  kikombe cha dhahabu, mipira 3 na fedha kiasi cha Tsh.300,000/= huku mchezaji bora akiwa ni Nusura Almasi aliyefunga magoli 140 tangu mashindano kuanza. Mshindi wa Pili ni Kivesa Sekondari wamepata mipira 2, jezi  na fedha kiasi cha Tsh.200,000/=. Mshindi wa tatu Kabuku Quens walipata mipira 2 na Tsh.100,000/=.

 Mashindano hayo ya fainali yalimalizika salama huku yakishirikisha Wilaya nzima , wananchi walihamsika  ambapo  viongozi mbalimbali wa ngazi ya Wilaya na Mkoa walishiriki  huku  mchezaji bora wa mpira wa miguu , Nguruko Machele kutoka Kurugenzi FC akipata zawadi ya kombe.


Image may contain: 3 people, people smiling, people sitting and crowd

Image may contain: 8 people, people smiling, crowd, shoes, child and outdoor

Shamra shamra za wachezaji wa mpira wa pete  kabuku quens

Image may contain: 6 people, people smiling, people standing and outdoor

Kaptaini wa timu ya Kurugenzi FC iliyoshika nafasi ya pili akikabidhiwa zawadi za mipira na Mbunge wa jimbo la Handeni Mji Mh. Omary Kigoda jana.

  Image may contain: 3 people, people smiling, people sitting


Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Tanga Bi. Aisha Kigoda akikabidhi zawadi kwa mwwalimu wa timu ya mpira wa Pete Kivesa sekondary kwa kuwa washindi wa pili.

Mchuano kati ya Wanawake live na Kivesa Sekondari ukiendelea.

Kurugenzi FC wakipambana na Vibaoni FC

Mwenyekiti wa CHANETA Wilaya Bi.Amina Kigoda akikabidhi zawadi kwa Mfungaji bora wa mpira wa pete Nusura Almasi, katikati ni  mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe.

Mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu Wilaya Bw.Essau Ngadala akikabidhi zawadi ya kombe la dhahabu kwa mchezaji bora wa mpira wa miguu Nguruko Machele kutokea Kurugenzi FC

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Bw Thomas Mzinga akikabidhi zawadi kwa washindi wa Uchumi Cup, kaptaini wa vibaoni akipokea.

Mkurugenzi Halmashuri ya Wiaya  ya Handeni Bw.William Makufwe akikabidhi Kombe la dhahabu kwa washindi wa mpira wa pete wanawake live, pembeni ni Mkuu wa Wilaya Mh. Godwin Gondwe.



Viongozi wakifatilia kwa makini mechi jana kwenye viwanja vya kigoda.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa