• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MASHINDANO YA UCHUMI CUP YENYE KAULI MBIU YA "KIPAJI CHANGU MTAJI WANGU" YAFUNGULIWA RASMI NA KUWATAKA VIJANA KUTUMIA VIPAJI VYAO KUKUZA UCHUMI

Imerushwa: February 5th, 2018

 Katika kuhamasisha vijana kujishughulisha na shughuli za maendeleo hususani kilimo  mashindano ya mpira wa mguu na mpira wa pete UCHUMI CUP yamefunguliwa rasmi kwa ngazi ya robo fainali na Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni mapema mwishoni mwa wiki.

 Akifungua mashindano hayo kwenye viwanja vya Kigoda Stadium  Kaimu Katibu Tawala Wilaya Bi.Upendo Magashi alisema kuwa michezo ni furaha na amani hivyo fursa hiyo itumike kukuza vipaji lakini pia kujiunga katika vikundi vya uzalishaji hususani kilimo ukizingatia Handeni shughuli kuu ni kilimo.

 Aliongeza kuwa lengo kuu la mashindano hayo ni kuhakikisha vijana wanatumia vipaji walivyonavyo katika kuhakikisha wanainua uchumi wao na  kuendana na falsafa ya Mh. Rais ya HAPA KAZI TU!.

 Kwa upande wake mratibu wa  mashindano Bw. Baraka Nkatura  alisema kuwa Mashindano yalianzishwa na Mkuu wa Wilaya Mh. Godwin Gondwe  na kuamua kuyatumia kwenye msimu huu wa kilimo ili  kuhamasisha vijana kutumia vipaji vyao kujiinua kiuchumi.

 “Tunaamini mbali ya kukuza mahusiano baina yetu, tutaweza kubadilishana uzoefu utakaotusaidia  kukuza vipaji vyetu na kujiinua kiuchumi” alisema Mratibu.

 Upatikanaji wa timu zilizoshiriki Robo fainali ulianzia ngazi ya Tarafa tarehe 20/11/2017 ambapo, Tarafa 7 zilishiriki kutoa  timu mbilimbili  zilizoingia kwenye robo fainali na timu 2 alikwa  moja kutoka jamii ya wamasai na ya pili kutoka  Kabuku. Jumla ya timu 18 zimeingia ngazi ya mashindano ya robo fainali.

 Aidha, baada ya kupatikana timu 18 kutoka kila Tarafa iliundwa mechi ya makundi  kwa timu za ( Mjini Chanika kundi  A, Misima B, Mkata C na Kabuku D). washindi wawili waliopatikana katika kila kundi waliingia robo fainali na kufanya timu shiriki 8.

 Mpaka tarehe 4/2/2018 timu 4 zimecheza robo fainali , mchezo kati ya kurugenzi Fc na Nyikani walitoana 2-1, Ambapo Kurugenzi FC  iliwafunga  Nyikani FC bao 2 kwa mojo. Dakika ya 5 mchezaji  John kutoka Nyikani FC alifunga goli la kuongoza na baadae  mchezaji Nguruko kutoka Kurugenzi FC alisawazisha goli dakika ya 30 kabla ya mapumziko. Mchezaji Peter aliifungia Kurugenzi FC kwa shuti nje ya 18 Dakika ya 70 na kufanya bao la pili.

 Mechi zinazocheza Robo fainali kwa lengo la kupata washiriki wa nusu fainali na fainali ni Kurugenzi FC vs Nyikani FC, Vibaoni United vs Kwamkono FC, Mtazamo United vs Ndolwa United na Umoja FC Vs Kwapara FC ambapo mwisho wa mashindano ya robo fainali ni 6/2/2018. Nusu fainali itachezwa tarehe 8-9/2/2018 na Finali itachezwa tarehe 11/2/2017.

 Mashindano haya yamebeba kauli mbiu ya “Kipaji changu mtaji wangu” mbapo Mshindi wa kwanza atapa zawadi ya Kombe, pesa taslimu Tsh.500,000/=,medali za dhahabu, jezi seti moja na mipira mitatu. Mshindi wa pili atapata pesa taslimu Tsh.300,000/=, medali za fedha(Silva), jezi seti moja, mpira mmoja. Na mshindi wa tatu  pesa taslimu Tsh.200,000/=,medali za shaba (Brons), jezi seti moja na mpira mmoja.

 Washindi wa mpira wa Pete , mshindi wa kwanza atapata fedha taslimu Tsh.500,000/=, mshindi wa pili Tsh.300,000/= na mashindi wa tatu Tsh.200,000/=.

Image may contain: 5 people, people standing and outdoor

Kaimu Katibu Tawala Wilaya Bi. Upendo Magashi Akifungua mashindano ya robo fainali kwenye viwanja vya kigoda jumamosi tarehe 3/2/2018 kwa kuhamasisha vijan kujiunga kwenye vikundi vya uzalishaji hususani kilimo.


Image may contain: 3 people, people standing and outdoor

Mratibu wa mashindano akizungumza  na wachezaji wakati wa ufunguzi wa mashindano ya robo fainali kwenye viwanja vya kigoda jumamosi 

Image may contain: 12 people, people smiling, people standing, sky, grass, outdoor and nature 

Timu ya Vibaoni United kabla ya kuanza mashindano dhidi ya Kwamkono united.


Image may contain: 12 people, people smiling, people standing, sky, outdoor and nature

Timu ya Kwamkono United katika picha ya pamoja kabla ya kuanza mchezo.

wachezeshaji wa mpira wakiwa katika picha ya pamoja na mratibu wa mashindano wa kwanza upande wa kulia Bw. Baraka Nkatula.


mapambano baina ya Vibaoni united na Kwamkono United yakiendelea viwanja vya Kigoda.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa