• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mbunge wa jimbo la Handeni vijijini akabidhi gari la wagonjwa kituo cha afya Kabuku.

Imerushwa: June 9th, 2020

Mbunge wa jimbo la Handeni vijijini Mh. Mboni Mhita akabidhi gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) kituo cha afya Kabuku. Amesema lengo la kuomba gari hilo kutoa msaada kwa wananchi kupelekwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kuitekeleza ahadi yake aliyoiahidi ya kuleta gari katika kituo cha afya Kabuku.

 Akitoa shukrani zake kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Mboni Mhita amempongeza Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni kwa kazi nzuri anayoifanya Handeni na ushirikiano wake na ofisi ya mbunge kwa kutekeleza vizuri ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Pia amempongeza kusimia suala la elimu Handeni kiwango cha elimu kimepanda mpaka kufikia 87% ya ufaulu kwa matokeo ya darasa la saba mwaka 2019.

Mh. Mboni Mhita amewashukuru wataalam wa Halmashauri ya Handeni kwa kusimamia fedha za maendeleo zinazoletwa kwenye Halmashauri na kuwapongeza wahudumu wa afya kwa kazi kubwa wanayoifanya. Amesema ameahidi kiasi cha milioni mia mbili (200M) kwaajili ya zahanati ya Segera na milioni mia nne (400M) kwaajili ya zahanati ya Kwamsisi.

Ameongeza  kuwa ameshawapata wadau wa Afya kutoka Marekani ambao watampatia kontena mbili za vifaa tiba kwaajili ya kusaidia wagonjwa wa Handeni.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. William Makufwe akimshukuru mbunge kwa kutekeleza majukumu yake kwa wananchi kwa kuleta gari la wagonjwa, amesema vituo vya afya nchi nzima ziko 352 na gari zilitolewa 50 hivyo ni juhudi kubwa iliyofanywa na mbunge mpaka kituo cha afya Kabuku kupata gari la wagonjwa.

Mh. Makufwe amesema kuwa walipata milioni mia nne (400M) kwaajili ya ujenzi wa majengo ya kituo cha afya Kabuku lakini wao kama Halmashauri wameongezea Milioni thelathini (30M) ili kuongezea umaliziaji wa majengo hayo. Pia Halmashauri wametoa kiasi cha Shilingi milioni hamsini na mbili (52M) kwaajili ya kujenga mifumo ya maji na kuweka umeme katika kituo cha afya Kabuku.

Alihitimisha kwa kusema kuwa Halmashauri imemepata milioni mia tano (500M) kwaajili ya umaliziaji wa jengo la hospitali ya Halmashauri inayojengwa Mkata na kwa bajeti ijayo tumetengewa kiasi cha bilioni 1.5 kwaajili ya hospitali ya Halmashauri na milioni mia tano hamsini (550M) kwaajili ya kujenga majengo katika kituo cha afya Kabuku.

Mganga mkuu wa kituo cha afya Kabuku Dr Lukas  Masele amemshukuru mbunge kwa kuona umuhimu wa kuleta gari la kisasa la kubebea wagonjwa kituo cha afya Kabuku pia amempongeza mkurugenzi mtendaji kwa kuwa msikivu kwa kutoa ushirikano wakati wowote unapohitajika.

Mbunge wa Handeni vijijini Mh. Mboni Mhita aliyesimama akiongea kwenye zoezi la kukabidhi gari kituo cha afya Kabuku.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe kulia akiwa pamoja na viongozi wa kata ya kabuku wakiomba dua wakati wa zoezi la kukabidhi gari.

Afisa utumishi wa Halmashauri ya Handeni Bi. Fatuma Kalovya akisisitiza jambo kwenye zoezi la kukabidhi gari.

Mganga mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Dr. Ipyana Mwandelile akitoa shukrani kwa mbunge kwa kupokea gari la kubebea wagonjwa Kituo cha afya Kabuku.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa