• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MH.RAIS MGUFULI AMETOA SIKU 15 KUCHUNGUZWA UBADHILIFU WA FEDHA ZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA HANDENI MKATA SHILINGI MILIONI 500

Imerushwa: August 2nd, 2017

Rais wa Jamhuri ya muungano wa TannzaKia Dk. Joseph Pombe Magufuli ametoa siku 15  kufanyika uchunguzi wa fedha kiasi cha shilingi milioni 500 zilizotolewa kwaajili ya ujenzi wa Hospitali ya Mkata kufuatiwa kuwepo na taarifa za kufuja matumizi ya fedha hizo.

Rais ametoa rai hiyo leo alipokuwa akizungumza na wananchi wa kata ya Mkata alipokuwa akipita kuelekea Tanga mjini kwenye ufunguzi wa Bomba la Mafuta.

Magufuli amesema kuwa uchunguzi ufanyike Haraka iwezekanavyo ili fedha nyingine Milioni 800 zilizotenga kwaajili ya kumalizia jengo hilo la Hospitali ziletwe na kufanyiwa kazi iliyokusudiwa.

Amesema kuwa ataendelea kutumbua majipu hususani kwa wale ambao wamezoea kuiba fedha za miradi ya wananchi hususani wannchi wanyonge na kwamba anataka watanzania wanyonge waweze kuifurahia nchi yao.

“Siku 15 jibu liwe limepatikana ili fedha nyingine zije, kama kuna mkandarasi hafai afukuzwe au mtu mwingine yeyote hafai  aondolewe ili tuanze ukurasa mpya , Mkuu wa Wilaya simamia hili kwa sababu lipo ndani ya uwezo wako”amesema Magufuli

.

Aidha Mh.Rais Magufuli amesema kuwa kuhusu suala la maji Serikali imeanza kushughulikia likiongozwa na wabunge wa majimbo ya Handeni, kiasi cha Bilioni 2 zimetolewa ili kuhakikisha kwamba tatizo la maji linakwisha na atahakikisha Mkata na Handeni wanaondokana na tatizo hilo.

 Sambamba na hilo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania leo amewarudishia wananchi wa Kata ya Kabuku ekari 50 za ardhi walizokuwa wamewapa JKT Mgambo zaidi ya miaka 10 kwaajili ya ujenzi wa Kiwanda ambacho  hakijaendelezwa, Amewataka JKT kujenga kiwanda ndani ya maeneo yao kwani wanayo maeneo makubwa yenye nafazi za kujenga .

 Mh. Raisi amewataka wakazi wa Handeni na Tanga kwa ujumla kujipanga kunufaika na fursa ya bomba la mafuta ili kuinua familia zao kiuchumi kwa kufanya kazi kwa juhudi, kulima mazao ya chakula  ya kutosha ,amehakikisha kuwa mradi huu utatoa  mchango mkubwa wa kimaendeleo kwa wananchi wa Tanga na Tanzania kwa ujumla.

 “ Wananchi na watani zangu Tanga inafunguka kiuchumi, nawahakikishia kwamba mradi huu ni mkubwa na utazidi kuinua uchumi wetu zaidi ya KM1000 zinajengwa ndani ya Nchi ya Tanzania tu, watu watafanya biashara, wananchi watapata vibarua na kazi za kudumu” Amesema Mh. Rais Magufuli.

Mwisho amewataka wananchi wa Tanga kudumisha ummoja na mshikamo kwa kuwatumia vizuri viongozi kwenye kuleta maendeleo na kuwataka vijana kuacha kutumika na watu wasiopenda kuona Tanzania inakuwa na amani, wasidanganywe na vitu vya bure kwani huu ni wakati wa kufanya kazi ili kuweza kupata fedha za halali na kwamba hakuna vitu vya bure.

Mh. Rais  Magufuli anatarajiwa kuweka jiwe la Msingi kwenye bomba la Mafuta linalotoka Uganda, Hoima hadi Bandari ya Tanga, Tanzania tarehe 5/8/2017,  Viongozi mbalimbali Waziri wa Afya,Ustawi wa jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mh.Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mh.Januari Makamba,Wabunge wa Handeni, Mkuu wa Mkoa wa Tanga na Mkuu wa Wilaya ya Handeniwalishiriki kwenye mikutano iliyofanyika Kata za Mkata, Komkonga, Kabuku na Segera (Michungwani) Wilayani.


Image may contain: 3 people, people standing, sky, crowd and outdoor

Kwa kwanza kushoto ni  Diwani wa Kata ya Mkata akifuatiwa na wakuu wa Idara wa Halmshauri ya Wilaya ya Handeni wakiongoza msafara njiapanda ya Handeni kumpokea Rais.

Image may contain: one or more people, people standing, people walking, car and outdoor 

Viongozi mbalimbali wakiwa tayari kumpokea Rais.

Image may contain: 2 people, people standing, sky, cloud, crowd and outdoor 

Diwani wa Kata ya Mkata akizungumza shida zake mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

  Image may contain: 4 people, crowd, sky and outdoor

Baadhi ya wananchi wliojitokeza kumlaki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Image may contain: 1 person, walking, standing, sky and outdoor 

Mbunge wa Handeni Vijijini Mh. Mboni Mhita akizungumza na wananchi wa Mkata.



















































































































Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa