• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI AAGIZA UADILIFI UAMINIFU NA UWAJIBIKAJI IWE NGUZO YA KUKUZA TAALUMA SHULENI

Imerushwa: February 21st, 2018

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe amewataka walimu,Wakuu wa shule za Sekondari na Walimu Wakuu wa shule za Msingi kufanya kazi kwa Uadilifu,Uaminifu na uwajibikaji ili kukuza taaluma  .

Ameyazungumza hayo jana  alipokuwa kwenye kikao kazi na walimu wa Kata ya Kwachaga kilichofanyika Shule ya Msingi Taula, chenye lengo la kuinua taalumu kwenye shule za Msingi na Sekondari kwa kujitafakari mahali taalumu ilipotoka, ilipo na inapoelekea .

Mkurugenzi amesema kuwa Serikali imewaamini na kuwapa dhamana waliyonayo hivyo ni vyema kusimamia vyema vizuri majukumu waliyopewa, alisema kuwa  walimu lazima wawe na nidhamu ya kazi  ili hata wanaofundishwa waweze kupata mifano kutoka kwa walimu wao.

“Walimu lazima muwe na malengo katika kazi zenu mbali na changamoto mbalimbali mazopitia, weledi wa taaluma na malengo yanayofikika , naamini walimu mnao uwezo wa kufanya taaluma ipande au ishuke”. Alisema Makufwe.

Aidha aliwataka wakuu wa shule na walimu wakuu ambao ni wajumbe kamili kwenye vikao vya maendeleo vya Vijiji(KAMAKA) kupeleka matokeo ya wanafunzi na kuweka agenda ya  kuinua taaluma kwa wananchi kama agenda ya kudumu  itakayojadiliwa na wananchi wote ili kujitathmini kwa pamoja na kuona maendeleo ya watoto wao hatimaye kurahisisha ushiriki wa jamii kwenye kuinua elimu na taaluma kwa ujumla.

“walimu mpeleke ripoti za watoro,matokeo ya majaribio na kitaifa na taarifa za maendeleo za shule za Msingi na Sekondari, taaluma izoeleke kama moja ya maendeleo kwa jamii na wazazi/walezi watatambua wajibu wao” alisema Makufwe .

Katika kuhakikisha watoto wanapata chakula shuleni Mkurugenzi ameataka walimu kuwashirikisha wanafunzi kwenye elimu ya kujitegemea (EK) kwa kulima walau ekari 2 za mazao ya mahindi, maharage na mbaazi , lengo likiwa ni kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula bila bugudha yoyote.

Wakati huohuo Mkurugenzi amewataka walimu kufuata miongozo na kuzingatia matumizi sahihi ya fedha za Serikali zinazoletwa kwaajili ya maendeleo ya shule na kusema kuwa  marufuku kubadili matumizi ya fedha na kwamba hatakuwa tayari kumvumilia yeyote atakayekwenda kinyume na maelekezo.

Mkurugenzi alisema ataingia mkataba na Maafisa elimu yenye lengo la kuongeza ufaulu kwa 30% na Maafisa elimu wataingia makubaliano na walimu katika kuhakikisha malengo yaliyokusudiwa yanafikiwa.

Ziara ya kikazi ya Mkurugenzi Mtendaji  na walimu, wakuu wa shule na walimu wakuu kwa Kila kata imenza jana na itaendelea kwa kata zote 21 katika kuhakikisha malengo ya;iyowekwa yanafikiwa na changamoto wazokabili walimu zinazoweza kutatuliwa na ofisi ya mkurugenzi zinatatuliwa kwa wakati.

Matokeo ya darasa la saba  Halmshauri ya Wilaya ya Handeni imepanda kutoka 62.3% mwaka 2016 hadi 72.55%  mwaka 2017 ambapo kitaifa imeshika nafasi ya 83 Kitaifa kati ya Halmashauri 186  na  nafasi ya 5 kimkoa kati ya Halmashauri 12.

Matokeo ya kidato cha nne Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imepanda kutoka 66% mwaka 2016 hadi kufikia 76% mwaka 2017 ambapo kimkoa imeshika nafasi ya 8 kati ya Halmashauri 12 na Kitaifa nafasi ya 155 kati ya Halmashauri 195.

 

Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe akiendelea kuzungumza na Walimu kwenye darasa la shule ya Msingi Tuliani.

baadhi ya waalimu

Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Kwachaga  Bi. Halima Salim akielezea changamoto zinazoikabili shule yake na  namna wanavyojipanga kuboresha taaluma.

Mkuu wa shule ya Sekondari Kwachaga Bw.Halid Ibrahimu akielezea changamoto za shule yake  kwa Mkurugeni na Maafisa Elimu.

Walimu wakisikiliza kwa makini maelekezo kutoka kwa mKurugenzi Mtendaji.

Mwalimu wa masomo ya Science shule ya Sekondari Kwachaga Bw. Jacob Onesmo akieleza  changamoto anazopitia ili kupatiwa ufumbuzi.

Afisa Elimu  Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  Bw. Fikeni Senzighe akifafanua baadhi ya maswali waliyouliza walimu waliyouliza  kwenye kipindi cha kusikiliza kero zao na changamoto


Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  Bw.Simoni Mdaki akifafanua maswali ya walimu waliyouliza ili kujua mustakabari wao.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa