• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkurugenzi afanya kikoa na wadau wa Muhogo.

Imerushwa: October 7th, 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. Saitoti Zelothe Stephen amekutana na kufanya kikao na wadau wa zao la Muhogo kwenye Halmashauri ya Handeni.

Wadau hao ni pamoja na Wakulima wa zao la Muhogo, Banki ya NMB, Taasisi ya utafiti wa mazao  jamii ya mizizi kutoka Kibaha (TARI), Taasisi inayosimamia mnyororo wa thamani wa uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora  za muhogo (MEDA), Taasisi ya Kilimo ya Kitaifa katika ukanda wa joto (IITA) na Kampuni ya Kibiashara ya kununua muhogo na kusafirisha nje ya nchi (Dar Kanton).

 Bw. Saitoti amesema biashara ya muhogo inahitaji uadilifu na uaminifu wa kila mtu kwa uapnde wake na Halmashauri inajukumu la kuhakikisha zao la muhogo liwe na manufaa kwa  Halmshauri na kwa  kila mkulima mmoja mmoja.

Kwa kumalizia Mkurugenzi Mtendaji Bw. Saitoti Zelothe Stephen ametoa maelekezo kwa wataalam wa sekta ya kilimo kwenda kwa wakulima kutoa elimu ya namna ya uchakataji wa muhogo kuanzia Jumamaosi ya tarehe 09/10/2021 ili kuongeza thamani kwaajili ya  kupata faida na kurejesha marejesho.

Afisa kilimo Wa Halmashauri ya Handeni Ndugu Yibalila Kamele Chiza amesema  muhogo ni zao moja wapo la kimkakati kwenye Halmashauri ya Handeni hivyo Halmashauri iliamua kutafuta mkopo ili kuwakopesha wakulima na vikundi 43 vya wakulima wa muhogo wenye watu zadi ya mia saba wamepata mkopo wa kilimo cha muhogo kwenye Halmshauri ya Handeni, sasa wanatarajia kuvuna na kuuza hivyo kubadilisha maisha ya wananchi wa Handeni kwa kuongeza kipato chao.

Kwa upande wa Meneja wa banki ya NMB Handeni Bw. Kilonzo amesema wao ni wadau wa kilimo cha muhogo na walishatoa mkopo kwa wakulima wa Handeni kiasi cha Bilioni 3.4 sasa  wanatoa fedha kwaajili ya kuandaa vifaa vya kukaushia muhogo ili wakulima kuongeza thamani ya mazao yao  kwaajili ya kupata faida na kurejesha marejesho.

Mnunuzi wa Muhogo kutoka Kampuni ya Kibiashara ya kununua muhogo na kusafirisha nje ya nchi (Dar Kanton)  amesema kuwa wako tayari kununua muhogo mkavu kutoka  kwa wakulima wa muhogo  wa Handeni na muhogo unaochakatwa  na maganda yake unahifadhika kwa muda mrefu.

Pia amesema wataleta mashine kumi na tano za  kuchakatia ili wakulima waweze kuchakata muhogo kwa haraka na watanunua muhogo kwa ujazo wa kilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. Saitoti Zelothe Stephen, akiwasikiliza kwa makini wakulima wa muhogo.

Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Handeni Ndugu.Yibalila Kamele Chiza akisoma taarifa ya zao la Muhogo kwenye Halmashauri.

Afisa Utumishi Bw. Maximillian Makota akiongea kwenye kikoa hicho.

Maafisa Mapato na Biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya  Handeni wakisikiliza maagizo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo.

Wadau wa zao la Muhogo kutoka benki ya NMB.

 Mnunuzi wa Muhogo kutoka kampuni ya Dar kantoni, akieleza jambo kwenye kikao hicho.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa