• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkurugenzi Mtendaji afanya kikao kazi na Watendaji Kata pamoja na Maafisa Elimu wa Kata.

Imerushwa: December 19th, 2022

Mtendaji  Kata ya Sindeni Bi. Amina Sakwalu pamoja na Afisa Elimu  wa Kata hiyo Mwl. Simon Charles wamepata zawadi ya fedha ya kiasi cha Tsh. 50,000 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. Saitoti Z. Stephen  kwa kufanya vizuri kwenye zoezi la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza kwa Mwaka wa masomo 2023 ambapo wameandikisha asilimia 120 ya matarajio waliojipangia.

Zawadi na pongezi hizo zimetolewa leo kwenye kikao kazi alichofanya Mkurugenzi Mtendaji kilichowashirikisha Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri pamoja na Watendaji wa Kata na Maafisa Elimu wa Kata zote 21 kwa lengo la  kupokea taarifa ya zoezi la uandikishaji kwa wanafunzi wa darasa la Awali na darasa la Kwanza.

Kwenye kikao hiko Mkurugenzi Mtendaji ametoa malekezo kwa Kata zote kuwa mpaka  kufikia tarehe 29/12/2022 ziwe zimefikia asilimia mia moja za uandikishaji huo.

Pia Bw. Saitoti Stephen amefuta likizo zote za maafisa hao na walioko likizo warudi mara moja ili washirikiane mpaka zoezi la uandikishaji litakapokamilika na Watendaji ambao hawatafikia asilimia mia moja ya uandikishaji atawapunguzia majukumu ya kazi yao au kuwapangia kazi nyingine.

Aidha ameagiza kwenda kuhamasisha zoezi zima la uandikishaji kwa jamii kwani elimu ni bure na kusisitiza kuwa siku ya kufungua shule masomo yaanze mara moja kwa wanafunzi waliopo na walioandikishwa.

Afisa Elimu ya Msingi Bi. Rehema Nyoka  amemshukuru Mkurugenzi kwa kufanya kikao kazi hiko na kuwataka maafisa hao kwenda kushirikiana na viongozi wa vijiji na vitongoiji ili wanafunzi waweze kupatikana  kwa wingi kwa ajili ya Mwaka wa masomo 2023.

Mkurugenzi Mtendaji Bw. Saitoti Z.Stephan (katikati) akiongoza kikao hiko.

Afisa Elimu Msingi Bi. Rehema Nyoka(kushoto) akiongea kwenye kikao hiko

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa