• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni afanya kikao cha hadhara na wananchi.

Imerushwa: August 19th, 2020

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe amefanya kikao cha hadhara na wananchi wa kijiji cha Taula kilichopo kata ya Kwedizinga ili kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi.

Bw. Makufwe amewashukuru wananchi wa kijiji cha Taula kwa kujitokeza na amewapa nafasi ya kueleza kero mbalimbali zinazowasibu kwenye kijiji chao kisha kuzitolea ufafanuzi. Akijibu na kuzitolea ufafanuzi kero za wananchi Mkurugenzi amesema Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imepeleka kiasi cha milioni sitini (Tsh.60M) shule ya sekondari Kwedizinga kwaajili ya ujenzi wa madarasa na miundombinu ya shule, pia imepeleka milioni arobaini na saba (Tsh.47M) kwaajili ya ujenzi wa madarasa na matundu ya vyoo kwenye shule ya msingi Taula na kiasi cha milioni arobaini na saba (Tsh.47M) kwaajili ya ujenzi wa madarasa na matundu ya vyoo kwenye shule ya msingi Ugweno.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni amesema kuwa za zahanati ya Taula itafunguliwa tarehe 26/08/2020 kwa kuwahudumia wananchi wa Taula na Handeni kwaujumla ameongezea kueleza kuwa hivi karibuni Halamshauri inatarajia kufungua zahanati ya Nkale iliyopo kata ya Kwamatuku, zahanati ya Kwamsangazi iliyopo kata ya Kwankonje na zahati ya Kwedikwazu iliyopo kata ya kwedikwazu ili ziweze kutoa huduma kwa jamii.

 Kwakumalizia Bw. Makufwe amesema kuwa viongozi kwenye Halmashauri yake waandae misaragambo ya miradi ya maendeleo na wampe taarifa atashiriki shughuli za maendeleo kwa vitendo kwa kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoka ofisini kwenda kushiriki shughuli za maendeleo kwa jamii.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. Wiliam Makufwe wa pili kushoto akisikiliza kero kutoka kwa mwananchi wa Kijiji cha Taula.

Mkurugenzi mtendaji Bw. Makufwe kushoto akitoa maelekezo kwa mwenyekiti wa kijiji cha Taula wakati akikagua jengo la zahanati ya Taula.

Afisa Utumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. Charles Mwaitege aliyevaa shati jeupe akisikiliza kero kutoka kwa wananchi.

Afisa mifugo wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. Sekiara N. Kiariro aliyeshika maiki akitoa ufafanuzi kwenye kikao hicho.

Wananchi waliojitokeza kumsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni na kutoa kero zao.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa