Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe jana ameongoza wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni pamoja na wananchi wa Mkata kufanya msaragambo wa kukarabati barabara inayotoka sheli ya Mogas kuelekea Mhalango zilipo ofisi za Halmashauri ya Wilaya Handeni.
Katika msaragambo huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni amewashukuru wafanyakazi wa Halmashauri hiyo pamoja na wananchi waliojitokeza kwenye zoezi la kurekebisha barabara hiyo.
Pia Mkurugenzi Mtendaji Makufwe amesema wameamua kutenga siku maalumu kutoka ofisini na kwenda kushiriki shughuli za kimaendeleo kwenye jamii.
Ameongeza kuwa zoezi la kutoka ofisini kwenda kushiriki shughuli za maendeleo kwenye jamii itakuwa endelevu kwa Halmashauri yake kwaajili ya maendeleo ya Taifa.
Kwaupande wa wafanayakazi wa Halamshauri ya Wilaya ya Handeni wameishukuru ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa kuamua kuirekebisha barabara hiyo kwani ilikuwa ni changamoto kupita kwenda ofisini hasa kwa vyombo vya usafiri.
MWISHO.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (C.C.M) Wilaya ya Handeni Mh. Athumani Malunda mwenye tisheti ya kijani akishiriki msaragambo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe aliyeshika chepe akitoa mchanga kwenye mtaro.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe akipokea viroba vilivyojazwa mchanga.
Afisa uchaguzi Bw. Francis Mashalo akibeba viroba vya vifusi kwenye msaragambo huo.
Wafanyakazi wa Halmashauri walijitokeza kwa wingi kwenye msaragambo wa kukarabati barabara
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa