• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI AMEWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHARI KATIKA KIPINDI HIKI CHA MVUA.

Imerushwa: May 10th, 2017

Wananchi Wilayani Handeni wametakiwa kuchukua Tahadhari ya Magonjwa ya mlipuko na madhira yanayoweza kujitokeza  kwenye kipindi hiki cha mvua.

Tahadhari hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauriya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe ofisini kwake jana alipokuwa akizungumza na wandishi wa Habari.

Mkurugenzi Mtendaji alisema kuwa mvua zinanyesha kwa mfululizo madimbwi na mabwawa yanajaa maji na wananchi wengi wanatumia maji hayo kwa kunywa bila kuyatibu hali inayoweza kupelekea magonjwa ya mlipuko hasa ukizingtia Halmashauri ya Wilaya ya Handeni inatatizo la  upatikanaji wa maji safi.

“ Wananchi wanao wajibu wa kulinda afya zao kwa kuwa makini na maji wanayotumia kwa kunywa na kupikia hasa ya kwenye mabwawa na madimbwi kwani maji hayo mara nyingi  huambatana na kubeba  uchafu unaopelekwa kwenye vyanzo vyetu vya maji” Alisema Makufwe.

Aidha, alitaka tahadhari hizo  kuchukuliwa kwenye maeneo ya shule kwa kuzingatia ubora wa madarsa hasa yale yaliyojengwa kwa udongo kuepuka madhira ya kudondokea wanafunzi, ni muhimu kuchukua tahadhari ya kuwahamisha mapema.

Aliwataka wazazi kuwa makini na watoto wao kwenye kipindi hiki cha mvua, Mito mingi inajaa na watoto huwa wanavuka maranyingine kwenda shule. Watoto waelekezwe maeneo salama ya kupita na kama kuna uhitaji wa watoto kuvushwa basi wazazi/walezi wawe tayari kuwasaidia watoto.

Aliwaasa wanachi waliojenga mabondeni, kwenye mikondo ya maji na sehemu hatarishi Mkurugenzi Mtendaji aliwataka kuchukua tahadhari ama kuhama kabisa kwenye maeneo hayo na kutoa rai kwa wananchi kuacha kujenga nyumba kwenye maeneo hatarishi.

Wakati huohuo aliwataka wakulima kutumia vizuri mvua hizi zinazoendelea kunyesha kwa  kulima na kupanda mazao yale yanayokomaa kwa muda mfupi na muda mrefu hasa kwa kuzingatia kipindi cha miaka miwili iliyopita hakukuwa namvua za kutosha.

“Handeni hatuna zao la biashara zaidi ya mazao ya chakula kama mahindi, wananchi wote wa Handeni na ambao mko nje ya Handeni karibuni mpande mikorosho ikiwa ni mtu mmoja mmoja au kikundi, ardhi ya handeni inaruhusu na tupo kwenye kampeni ya kuhamasisha upandaji wa zao la biashara la korosho” Alisema Mkufwe.

Aliongeza kuwa korosho ikilimwa itaongeza na kuimarisha uchumi wa Handeni, lengo likiwa ni kusaidia kuelimisha jamii ya Handeni kwamba yapo mazao zaidi ya Mahindi ambayo yanaweza kuinua uchumi wa Halmashauri yetu.

Kwa upande wa agizo la Mkuu wa Mkoa la kupiga marufuku uuzaji wa mahindi mabichi Mkurugenzi Mtendaji amesema atahakikisha anasimamia kwa kushirikiana na Maafisa watendaji Kata na  Vijiji kwani Halmashauri bado haijatambua kama kutakuwepo na mahindi ya ziada baada ya mavuno licha ya mvua ambazo bado zinaendelea kunyesha. Lengo ni kudhibiti upungufu wa chakula unaoweza kujitokeza hapo baadae na hatua za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayekwenda kinyume na tamko hilo.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa