• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa mkoa ashiriki kikao maalum cha baraza la kujadili hoja za mkaguzi wa hesabu za serikali.

Imerushwa: June 8th, 2020

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Handeni limefanya kikao cha ukaguzi ili kujibu hoja za mkaguzi mkuu wa Serikali. Kikao hicho kimeudhuliwa na Mkuu wa mkoa, katibu tawala, mkaguzi mkazi wa mkoa wa Tanga, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Handeni, Mkuu wa wilaya ya Handeni pamoja na kamati ya ulizi na usalama ya wilaya ya Handeni.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Handeni Mh. Mustapha Beleko, amemshukuru mkuu wa mkoa pamoja na viongozi alioambatana nao kutoka mkoani kushiriki kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Handeni. Mh Beleko amesema kuwa baraza la madiwani la Handeni  linashirikiana vizuri na  viongozi wa mkoa na wilaya na kutimiza ilani ya Chama Cha Mapinduzi  kwa maendeleo ya Taifa na Handeni kwaujumla.

Mkuu wa mkoa wa Tanga  Mh.  Martine Shigela aliwapongeza baraza la madiwani kwa kazi nzuri wanayofanya na kupokea maelekezo ya serikali na kuipaisha Handeni  kimaendeleo. Pia amewapongeza wafanyakazi wa Halmashauri ya Handeni kwa kuitikia maagizo ya Mheshimiwa Rais ya Halmashauri zote zilizokuwa zinakaa mjini kuhama na Handeni imefanya hivyo mara baada ya kupata maagizo hayo.

Mh. Martine Shigela amewapongeza Mkuu wa Wilaya ya Handeni pamoja na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Handeni kwa kuhakikisha muhogo unalimwa kwa wingi Handeni na pia wanafunzi wa shule zote wanakula  chakula cha mchana kwa kutumia vizuri elimu ya kujitegemea.

Mkuu wa mkoa huyo amewakumbusha madiwani kubuni vyanzo vingi vya mapato ili kuongeza ukusanyaji wa mapato Handeni. Mh. Shigela amewakumbusha watalamu wa ardhi wa Halmashauri  kuwa viwanja vipimwe na viuzwe ili Halmashauri kujiongezea mapato kutokana na uuzwaji wa viwanja.

Katibu tawala mkoa wa Tanga Bi Judica Omary amewaeleza baraza la madiwani kuwa mipango inayopangwa kwaajili ya maendeleo ya Halmashauri ifuatiliwe na iwe ya kutekelezeka kwa haraka. Pia amewakumbusha madiwani kuwafuatilia wanafunzi wa kidato cha sita waliotangaziwa kufunguliwa kwa shule wanarudi haraka shuleni kwaajili ya kwenda kujiadaa na mitihani yao.

Mwenyekiti  wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Handeni Mh. Athumani Malunda amesema ukaguzi wa ndani ufanyike mara kwa mara kabla ya wakaguzi wan je kuja kukagua. Aidha amesema  kuwa vikundi vyote vilivyokopeshwa virejeshe pesa ili wengine nao waweze kukopeshwa.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe kwa upande wake amewapongeza madiwani kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kusimamia ujenzi wa madarasa katika kata zao na kuifanaya  Halmashauri ya Handeni kuongoza kwenye ujenzi wa maboma kwa mkoa wa Tanga.  

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. Williamu Makufwe amemshukuru mkuu wa mkoa pamoja na wageni alioambatana nao kwa kushiriki kikao cha baraza la madiwani la Handeni.

 Bw. Makufwe alimuahidi mkuu wa mkoa kuwa  maelekezo yote yaliyotolewa yatafanyiwa kazi hasa kuangalia vyanzo vipya vya ukusanyaji wa mapato. Pia suala la zao la mkonge amesema Halmashauri itaanzisha vitalu cha miche ya mkonge na kugawa miche hiyo kwenye shule za Halmashauri ya Handeni ili kuunga mkono juhudi za elimu ya kujitegemea hatimaye shule ziongeze mapato.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Mustapha Beleko  aliyesimama akifungua kikao na kuwakaribisha wajumbe wa kikao hicho.

Mkuu wa mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigela akifafanua jambo kwenye kikao hicho.

Katibu tawala mkoa wa Tanga Bi. Judica Omary akisisitiza jembo kwenye kikao maalum cha baraza kujadili hoja za mkaguzi.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe akiongea kwenye kikao  hicho.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni aliyesimama akitoa ufafanuzi kwenye kikao maalum cha baraza kujadili hoja za mkaguzi wa hesabu za serikali.

Madiwani wa Halmashauri ya Handeni wakiwa kwenye kikao maalum cha kujadili hoja za mkaguzi wa hesabu za serikali.

Mkaguzi wa ndani wa Halmashauri ya Handeni Bw. Saturine J. Kessy aliyesimama akisoma hoja zilizojitokeza kwenye kikao hicho.

Mkuu wa mkoa Mh. Martine Shigela wa pili kushoto waliokaa akiwa na wafanyakazi wa Halmashauri ya Handeni.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa