• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa mkoa azindua huduma ya kituo cha kuuza mafuta Handeni.

Imerushwa: June 11th, 2020

Kituo hicho cha kuuza mafuta kinachomilikiwa na Serikali kupitia  Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzani (TPDC)  kinachoitwa TANOIL kilichopo michungwani kata ya Segera kimezinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga  Mh. Martine Shigela.

 Mkuu wa Mkoa amempongeza Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania kwa juhudi kubwa anayoifanya kwa kuleta maendeleo kwa wananchi  na namna alivyoweza kuongoza mapambano dhidi ya ugonjwa wa CORONA (COVID 19).

 Pia amempongeza  Mkurugenzi  mkuu  wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania  (TPDC) kwa kurudisha mali za serilaki zilizokuwa zinamilikiwa na watu binafsi na kuwashawishi wawekezaji kujenga bomba la mafuta kutoka Uganda Mpaka Tanga.

Mh. Martine Shigela amesema Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania wamefanya kazi nzuri ya kutafiti, kuchimba na kusambaza gesi  kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam na sasa wameanza kutoa gasi kutoka Dar es Salaam kwaajili ya kusambaza mkoa Tanga ili wananchi waweze kuitumia.  

Kwakuhitimisha amewakumbusha wafanyakazi wa Serikali na wananchi kwa ujumla kuwapa ushirikiano Shirika la Maendeleo  ya Petroli  Tanzania kutimiza malengo yao kwa wananchi na faida itakayopatikana itarudi kwa jamii  kujenga miundombinu mbalimbali.

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Dr. James  Mataragio amemshukuru  Mh Rais kwa kuiwezesha TPDC kurejea kufanyakazi kama hapo awali kipindi cha awamu ya kwanza pia amemshukuru mkuu wa mkoa wa Tanga kwa kushirikiana na TPDC kwenye miradi yake inayoitekeleza mkoa wa Tanga.  Amesema kuwa  Shirika litasimamaia usambazaji wa wa uhakika wa mafuta na kwamba  watajenga matenki makubwa ya kuwehifadhia mafuta maeneo ya Dar es Salaam, Morogoro, Tanga na Makambako ili wafanyabiashara waweze kuchukulia mafuta karibu na mazingira yao na  kwa kipindi cha miaka mitano ijayo watajenga vituo 100 vya mafuta nchi nzima ili kupeleka huduma kwa jamii.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni  Mh. Gondwin Gondwe ameshukuru mkuu wa mkoa kwa kuja kwenye halfa hiyo na kumueleza kuwa wananchi  wa Misima wameupokea mradi mkubwa wa bomba la mafuta na wamekubali kuupisha uwekezaji wa bomba la mafuta pia amesema wawekezaji waweze kupitia kwa wakurugenzi na kwa katibu tawala ili wananchi waweze kupata matunda ya uwekezaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni  Bw. William Makufwe amewashukuru TPDC kwa kuja kuwekeza Handeni na ametoa  eneo la kujenga sheli nyingine kwa  Shirika la maendeleo ya Petroli Tanzania bure  katika kata ya Mkata  ambako zipo ofisi za makao makuu ya Halmashauri ya Handeni ili wafanyakazi na wananchi wa Handeni  waweze kufaidika na uwekezaji huo.

Mkuu wa mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigela akijaza mafuta kwenye gari ishara ya kufungua kituo hiko.

Mh. Martine shingela wa tatu kushoto akimsikiliza mwananchi mara baada ya kufanya uzinduzi.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Gondwin Gondwe aliyeshika maiki akiongea kwenye uzinduzi huo.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania Dr. James Mataragio aliyeshika maiki akiongea kwenye uzinduzi huo.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. William Makufwe aliyesimama kushoto akitoa ufafanuzi wa kutoa eneo kwa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania bure ili wajenge sheli.

Wananchi waliojitokeza wakimsikiliza mkuu wa mkoa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa