• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Mkoa wa Tanga afanya kikao na Wananchi na Kukagua Miradi Msomera.

Imerushwa: January 23rd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Omary T. Mgumba amefanya kikao na wananchi wa Kijiji cha Msomera kisha kufanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali kwenye Kijiji hicho.

Baada ya kusikiliza changamoto na kero mbalimbali kutoka kwa wananchi Mkuu wa Mkoa amesema kuwa,eneo la Msomera ni pori tengefu na eneo la serikali hivyo kwa yeyote aliyekuwa anaishi huko yuko kinyume cha sheria na alikuwa ni mvamizi kama wavamizi wengine wa maeneo tuliyotenga.

Mhe. Mgumba amesema kuwa maeneo yote yaliyotengwa kwa ajili ya huduma za jamii kama vile barabara,shule au malisho yaendelee kubaki wazi kama yalivyopangwa na amewaomba wananchi waheshimu mipango ya Serikali kuepusha migogoro isiyofaa.

Pia amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji  Halmashauri ya Handeni kuwahamisha watu wote waliolima kwenye maeneo ya malisho au barabara kwa kupewa heka tano tano kwa ajili ya kilimo kwenye maeneo yaliyopangwa kwa ajili ya kilimo na kusimamia matumizi bora ya ardhi kama ilivyoelekezwa kisheria.

Katika ziara yake ya kukutana na wanachi wa Kijiji cha Msomera Mkuu wa  Mkoa pia alitembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotelezwa ambapo ni pamoja na ujenzi wa kituo cha Afya Msomera, ujenzi wa mnada na Ujenzi wa bwawa la maji linalosimamiwa na wakala wa usambazaji maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) na amehimiza miradi hiyo ikamilike kwa haraka ili iweze kutoa huduma kwa wananchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. Saitoti Stephen amesema kuwa anawashukuru wananchi wa Msomera kwa kuitikia suala la Eimu mpaka sasa uandikishaji umefikia zaidi ya 100% na changamoto ya umbali wa Kwenda shule kutoka katika  kitongoji cha Mkababu Halmashauri imedhamiria kujenga shule ili wanafunzi waweze kupata elimu kwa ukaribu zaidi.


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Omary Mgumba, wa pili kushoto aliyeshika karatasi akisikiliza taaarifa ya Kituo cha Afya Msomera kutoka kwa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Handeni Kulia.

Mkuu wa Mkoa akiendelea kukagua ujenzi wa Kituo cha Afya Msomera.

Katibu tawala Mkoa wa Tanga Bi. Pili Mnyema, aliyesimama akiongea kwenye kikao Hicho.

Afisa Tawala wa Wilaya ya Handeni Bi. Upendo Magashi, aliyesimama akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Handeni akiongea kwenye kikao hicho.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni Bw. Saitoti Stephen akiongea kwa kujibu changamoto za wananchi wa Msomera.

Wakuu wa Idara kutoka Halmashauri ya Handeni wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Tanga.


Wananchi  wa Kijiji cha Msomera waliojitokeza kumsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa