• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA WA TANGA AMEITAKA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI KUFUATA TARATIBU ZA MANUNUZI KUEPUKA HOJA ZINAZOWEZA KUZUILIKA

Imerushwa: July 2nd, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martin Shigella ameipongeza Halmashauri ya Wiaya ya Handeni kwa kuwa na hati safi na kuwataka  kufuata kanuni za manunuzi na kuweka kumbukumbu sahihi ili kuepuka kutengeneza hoja zinazoweza kuzuilika.

Ameyazungumza hayo  alipokuwa kwenye kikao cha Baraza la Hoja la CAG kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni mwishoni mwa wiki .

Mkuu wa Mkoa amesema kuwa manunuzi yote yanayaofanyika yanapaswa kuwa na vielelezo halali ili kuepuka kutengeneza hoja ambazo zingeweza kufutika, hoja ya kukosekana kwa vielelezo Halmashauri ichukue hatua kwa watendaji watakaohusika ambao wanatumia mianya kujinufaisha wenyewe.

Ameongeza kuwa fedha zinazoletwa ni muhimu zikatumika kwa wakati kwani mahitaji ya wananchi ni mengi na makubwa ili kuepuka bakaa, zibaki fedha ambazo hazikuletwa kwa wakati hivyo kuchelesha matumizi yake, fedha ambazo kwa wakati huo ndio Halmashauri imetangaza zabuni na sio sababu ya kushindwa kutumika.

“wekeni utaratibu wa kuhakikisha kila vikao mnavyokaa hususani kamati ya fedha mnajadili kiasi cha fedha kilichopo kila kwenye akaunti ili kujua matumizi yake kuepuka bakaa zinazoweza kuzuilika, wananchi wanahitaji kuhudumiwa kwa fedha hizo zinazoletwa na Serikali” Amesema Shigella.

Amesema kuwa hoja za malipo kwa watumishi hewa zisijirudie kwa kuhakikisha watumishi wote wanaokuja wanahakikiwa na kulipwa fedha kwa uhalali.

Kwa upande mwingine Katibu Tawala Mkoa Bi. Zena Said amesema kuwa fedha za mifuko ya afya CHF na NHIF hazitakiwi kupita mwaka labda ziwe zimechelewa kuletwa.

Madai ya watumishi  kutokuwa na uhalisia ameishauri Halmashauri kuhakikisha madai ambayo watumishi wanayadai kwa Serikali kuwa yamethibitishwa uhalali wake na kuonesha ushaidi na kuondoa dhana ya kufikiri Serikali inafedha nyingi kwaajili ya malipo hayo.

Mwenyekiti wa Wilaya ya Handeni Mh. Ramadhani Diliwa ameshukuru Mkuu wa Mkoa na timu nzima kutoka Mkoani kwa kushiriki pamoja na Halmashuri na kuahidi kusimamia utekelezaji maagizo yote yaliyotolewa kuepuka hoja zinazoweza kuepukika.


Mkaguzi wa ndani Bw. Saturine Kessy akiwasilisha hoja wakati wa kikao.

Baaadhi ya Waheshimiwa Madiwani na wataalamu mbalimbali wakisikiliza kwa makini maoni ya CAG

Waheshimiwa Madiwani katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 03, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa