• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WA WILAYA YA HANDENI AZINDUA RASMI ZOEZI LA USAJILI, UTAMBUAJI NA UFUATILIAJI WA MIFUGO( KUPIGA CHAPA)

Imerushwa: November 16th, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Handeni  Mh. Godwin Gondwe amezindua rasmi zoezi la Utambuzi,Usajili na Ufuatiliaji wa mifugo na kuwataka wafugaji kufuat sheria za kuingia mifugo mipya kwenye maeneo yao ili kubaini idadi halisi ya mifugo kuligana na rasilimali zinazohitajika kwenye uendelezaji wa mifugo.

Akizungumza na wafugaji kwenye uzinduzi wa zoezi hilo Mkuu wa Wilaya amewaeleza kuwa,  sheria zimewekwa ili kuwatumikia wananchi na kwamba kwa kuitikia wito wa kupiga chapa ya utambuzi wa mifugo yao ni kuunga mkono Serikali  kwa sababu zoezi hilo limelenga zaidi kuwalinda wafugaji.

Aliongeza kuwa kwa kupiga chapa mifugo kutasaidia kwenye suala zima la  ulinzi na usalama kwenye Wilaya ya Handeni  kwa kutambua mifugo ya kila mtu na kjiji itakayosajiliwa  hivyo kuwa na ulinzi mzuri.

 Amesema kuwa zoezi hili la utambuzi, usajili na ufuatiliaji wa mifugo lina faida nyingi ikiwemo kudhibiti wizi wa mifugo, kuzuia na kudhibiti kuenea kwa magonjwa ya mifugo kwani hakuna mfugo utakao ruhusiwa kuingia Wilayani Handeni pasipo kupimwa na kuboresha koosafu za mifugo  hali itakayopelekea kuwa na begu nzuri za mifugo hatimaye kuongeza fursa ya soko la uhakika kutokana na ubora wa mifugo.

Aidha aliwataka wafugaji na viongozi ngazi ya Vijiji kuwa makini na mifugo inayoingia kwenye maeneo yao kwa kuangalia uwiano wa mifugo waliyonayo na malisho, kwani kwa kukaribisha wafugaji wengine kiholela kutawapelekea wazawa kukosa maeneo ya malisho  na kwamba wasiwakaribishe bila kujiridhisha uwepo wa maeneo ya kutosha kwa kupitisha barua ya mwombaji kwa Uongozi wa Vijiji, baraza  la ardhi na mikutano mikuu ya wananchi.

“ lazima mtambue  na kusimamia sheria Na.12 ya malisho na maliasili ili muweze kulinda rasilimali za wanyama, idadi ya mifugo lazima iwe na uwiano na malisho, kuwa na mifugo mingi  mtakosa malisho Handeni na mkienda kuomba Halmashauri nyingine mtakosa”Alisema Mkuu wa Wilaya.

Aliongeza kuwa  akitokea mtu yeyote ambaye wananchi hawamfahamu  ataingiza mifugo kwenye maeneo yao bila kufuata sheria  watoe taarifa haraka iwezekanavyo kwani upigaji chapa ni muhimu na viongozi wapo kuhakikisha wanasimamia haki za wafugaji.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe  alisema kuwa kwa kufanya zoezi la upigaji chapa wa mifugo ni kutekeleza agizo la Serikali ambalo liliwataka Halmashauri kusimamia  na kuwataka wafugaji kutoa ushirikiano wao ili kufanikisha zoezi hilo kama ilivyokusudiwa.

Mkurugenzi Alisema kuwa mbali na kuitikia agizo la Serikali lakini zoezi hilo litasaidia kupunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji,kuepusha muingiliano wa mifugo baina ya Vijiji na Wilaya  na kubainisha kuwa zoezi hilo ni endelevu na hadi kufikia mwezi Desemba Kata 21 na Vijiji vyote 91 viwe vimefikiwa.

“Ng’ombe ambazo zitakuwa hazijapigwa chapa na kuingia kwenye maeneo ambayo hayaruhusiwi watapigwa mnada, naomba tusifike huko, leteni mifugo yenu ipigwe chapa  baada ya Desemba mifugo yote ambayo haijapigwa chapa itapigwa faini, sitaki  tufike huko” alisema Mkurugenzi

 Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Inatarajia kupiga chapa mifugo zaidi ya  lakimoja na elfu thelathini(130,000) ambapo uzinduzi umefanyika kwenye Vijiji vya Sua na Mazingara na Ng’ombe zaidi ya 932 wamepigwa chapa.





Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa