• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Handeni afanaya kikao kazi na walimu wa Handeni Vijijini.

Imerushwa: July 1st, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Godwin Gondwe amefanya kikao kazi na maafisa elimu wa sekondari na msingi, maafisa elimu kata pamoja na wakuu wa shule wa sekondari na msingi zote za Halmashauri ya Handeni lengo ni kupanga  malengo ya ufaulu wa wanafunzi mara baada ya kuisha kwa ugonjwa wa Korona na kufanaya tathmini ya namna walivyokuwa wanafundisha wakati wa likizo.

Mara baada ya kufungua kikao hicho Mhe. Godwin Gondwe alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni kwa kuwajali watumishi hususani kusimamia maslahi ya walimu pia aliwapongeza walimu kwa kufanya kazi kwa ushirikiano na kuiwezesha Halmashauri ya Handeni na kupanda kielimu mwaka hadi mwaka na matokeo ya darasa la saba mwaka 2019 yamepanda hadi kufikia 89% na kuwa Halmashauri ya 3 kati ya 11za kielimu zilizopo mkoa wa Tanga na  kusema kuwa umoja wetu ndiyo ushindi wetu.

Kwakuhitimisha Mhe. Godwin Gondwe amewaagiza maafisa elimu wa sekondari na msingi kusimamia nidhamu za walimu na kuwahi kazini na kuhakikisha kuwepo kwa vifaa vya kujikinga na ugonjwa wa Korona kama vile maji tiririka na sabuni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe alimshukuru mkuu wa wilaya kwa kufanya kikao kazi na walimu na kuwapa maelekezo baada ya likizo ya korona.

 Bw. William Makufwe amemueleza mkuu wa wilaya ya Handeni kuwa mwaka huu Handeni itakuwa ya kwanza kimkoa kwa matokeo ya mitihani ya Taifa na amewaeleza walimu kuwa malengo ya ufaulu yawe pale pale kwa 100% kwa darasa la nne, darasa la saba na kidato cha pili  na 90% kwa kidato cha nne.

Pia  amewakumbusha maafisa elimu kusimamia nidhamu za walimu na ruhusa zote za walimu zitatolewa na ofisi ya mkurugenzi ili kudhibiti utoro wa walimu.

 Kwakuhitimisha Mkurugenzi Mtendaji wa Handeni amesema kila mmoja awajibike kwa nafasi yake kusimamia na kufuatilia maagizo yote na ametoa lita 20 za mafuta kwa kila afisa elimu kata kwa kata zote za Halmshauri ya Handeni ili kwenda kukagua maagizo kama yanatekelezwa ipasavyo.

 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Godwin Gondwe aliyesimama akiongea na walimu wa Halmashauri ya Handeni. 

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe aliyesimama akisisitiza jambo kwenye kikao hicho.

Wakuu wa shule za sekondari na za msingi wakimsikiliza mkuu wa Wilaya ya Handeni.

 Baadhi ya wakuu wa shule za sekondari na za msingi wa Halmashauri ya Handeni wakipokea maelekezo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa