• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Handeni afanya kikao na Asasi za kijamii zilizoko Handeni.

Imerushwa: May 16th, 2018


Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe ameita Asasi za kijamii zilizoko Handeni ili kufanya kikao cha pamoja ambaye aliwakilishwa na Bw.William Makufwe Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni  jana katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya lengo likiwa ni kujua shughuli wanazofanya ili  kuepuka wadau hao kufanya mradi moja katika eneo moja na kuweka maazimio ya pamoja.Mashirika hayo ni AMREF, CAMFED , WORLD VISION , AGPAHI, ICAP, VISION FUND, DSW ,TAWOREK, NUYAMATA na NALIDO ambazo zinahusika nakusaidia pamoja kutoa elimu kwa jamii

Wakati wa ufunguzi wa kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmasahuri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe amesema mashirika hayo yanatakiwa kufanya kazi kwa kushirikiana na Halmashauri kwa kuziripori shughuli wanazofanya pamoja na kwamba kila shirika linaripoti katika maeneo lake ili Halmasahuri inapoandaa ripoti zake iweze kujumuisha taarifa za shughuli hizo kwa pamoja.

Amewaeleza wadau hao kuwa washirikishe Halmashauri  mafanikio na changamoto zinazopatikana katika jamii ili tutatue kwa pamoja na mwisho wa siku tutoke kwenye hatua moja kwenda hatua nyingine na kwamba kila moja atoe mawazo yake,  Pia amewasihi kuendelea kuisaidia Halmashauri kwa kutoa elimu kwa jamii kutatua matatizo mbalimbali kupitia misaada kutoka kwa wafadhili kwani Halmashauri inaupungufu mkubwa wa rasilimali.

Amehitimisha kwa kuwataka wadau kuweka maazimio ya pamoja baada ya kusahuriana ili kuweza kufanikisha mikakati ya kuitoa jamii kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine, Maazimio hayo ni kuwa shirika la DSW na CAMFED  waangalie utaratibu wa kuwasaidia vijana wa kiume wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwawezesha shughuli za kiuchumi kwani mashirika hayo misaada yao imeelekezwa kwa vijana wa kike zaidi.Shirika la WORLD VISION na CAMFED kukaa pamoja na kuona namna ambavyo wanaweza kufanya mafunzo kwa ushirikiano.

Pia amemtaka mwakalishi wa shirika la walemavu kupata taarifa ya walemavu wanaonyanyaswa hasa wanawake waliopewa mimba  na kufikisha ofisi ya Mkurugenzi. Amewataka wadau kutoa taarifa zenye takwimu ya kile kilichofanyika na mafaniko kwenye vikao vya wadau.

Ameongeza kuwa Mashirika binafsi yatoe taarifa ya utekelezaji wa shughuli za miradi yao kila baada ya miezi mitatu na Shirika la ICAP kuboresha huduma ya kubadili tabia kwa vijana baada ya kupima magonjwa ya zinaa hasa UKIMWI.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa