• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Handeni afunga rasmi mafunzo ya Jeshi la akiba

Imerushwa: December 4th, 2019


Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe amefunga rasmi mafunzo ya jeshi la akiba jana katika viwanja vya Kata Kabuku ndani Wilayani Handeni Mkoani Tanga ambapo mafunzo hayo yalianza  mwezi wa 01/08/2019.

Akifunga mafunzo hayo Mh. Gondwe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo alizitaka Taasisi za Serikali na Makampuni mbalimbali yaliyoko ndani ya Wilaya ya Handeni kuhakikisha wanawaajiri watu waliopitia jeshi la akiba na amesema ni marufuku Taasisi na Makampuni hayo kuajiri watu ambao hawajapitia jeshi la akiba.

Aidha ameipongeza Kampuni ya katani (KWALAGURU ESTATE) kwa kuwachukua jeshi la akiba 54 kati ya 60 waliohitimu jana na kuwataka Maafisa Tarafa kufuatilia makampuni mengine ili wale sita waliobaki waweze kupata ajira na amesema haiwezekani wengine wanapitia mafunzo ya jeshi la akiba lakini wengine ambao hawajapitia mafunzo hayo wanapatiwa ajira katika makampuni na Taasisi za Serikali.

Alihitimisha kwa kuwasihi wananchi kujiunga bima ya matibabu iliyoboreshwa (ICHF) shilingi 30,000 kwa watu 6 ambao watatibiwa mwaka mzima katika Hospitali za Wilaya, Vituo vya afya na Zahanati zote ndani ya Mkoa wa Tanga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe alimuahidi mgeni rasmi kuwaajiri watu waliopitia jeshi la akiba katika Ofisi zote za Halmashauri ya Wilaya ya Handeni. Pia alitumia nafasi hiyo kuwasihi wananchi kujikita katika shughuli za kilimo ikwepo Mihogo na Korosho ili kuondokana na njaa na umaskini.

Meja Donatus Tumaini Mashauri akisoma taarifa amesema kundi la 49 ilianza  mafunzo ya awali tarehe 1/08/2019 na kufunguliwa rasmi mwezi wa 9/2019 ambapo walikuwa wanafunzi 71 kati ya hao wakike 14 na wakiume 57 lakini hadi kufikia tarehe ya kuhitimu walibaki 60 ambapo 9 walishindwa mafunzo na 2 walifukuzwa kutokana na utovu wa nidhamu.

Aidha amesema lengo la mafunzo ya jeshi la akiba ni kuwaanda kwaajili kazi ya ulinzi na usalama ya Taifa bila woga, kushiriki katika mapambana na maafa yanapotokea, kushiriki katika gwaride na kushiriki katika ulinzi wa wananchi na mali zao pamoja na mipaka ya nchi.

Wahitimu wa mafunzo ya jeshi la akiba Elizabeth Paskali na Emanueli Masongo wamesema mafunzo yalikuwa magumu kiasi kwamba wengine walishindwa kumaliza lakini wanashuru wao kumaliza salama hivyo wanawaomba viongozi mbalimbali kuwaajiri jeshi la akiba katika Taasisi zao.



Imeandaliwa na;

Paulina John.

Kitengo cha Habari na mawasiliano Handeni DC


Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe akitoa hotuba kabla ya kufunga mafunzo ya jeshi la akiba

Meja Donatus Tumaini Mashauri akisoma taarifa ya mafunzo ya jeshi la akiba kundi la 49

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe akizungumza


Jeshi la akiba wakiwa kwenye gwaride wakimwonyesha mgeni ukakamavu wao

Jeshi la akiba kundi la 49 wakila kiapo 

Wananchi walijitokeza kushuhudia ufungaji wa mafunzo ya jeshi la akiba kundi la 49


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa