• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA YA HANDENI AMEMPA SIKU 90 MWEKEZAJI KIJIJI CHA MKOMBA KUFIKISHA HATI MILIKI YA ARDHI NA KUMPIGA MARUFUKU KUFANYA SHUGHULI ZOZOTE KATIKA ENEO HILO.

Imerushwa: July 31st, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe amempa siku 90 mwekezaji anayejulikana kama Hiragro LTD kufikisha hati ya kumiliki ardhi lenye ukubwa wa ekari1000 na kumpiga marufuku kufanya shughuli zozote mpaka atakapokamilisha taratibu za umiliki halali wa ardhi,kinyume na hapo ardhi itarudishwa kwa wanakijiji kwa kushindwa kuendeleza eneo hilo kama walivyokubaliana.

 Kauli hiyo ameitoa leo alipokuwa kwenye kikao baina ya wanakijiji wa Kijiji cha Mkomba kilichopo Kata ya Kwachaga Wilayani Handeni na wawekezaji wa Hiragro LTD ambao waliuziwa eneo hilo mwaka 2013, baada ya wawekezaji kukiuka makubaliano na kuanza kukata miti kwa kuvuna mbao,magogo na kuchoma mikaa kinyume cha makaubaliano.

 Mkuu wa Wilaya ameeleza kuwa ndani ya siku 90 kama hatafikisha hati miliki kwenye ofisi ya Mkurugenzi , ardhi hiyo itafanyiwa utaratibu kurudishwa kwa Mkurugenizi Mtendaji  ili wapangie mpango bora wa matumizi ya ardhi kwa manufaa ya Kata na Kijiji kwa ujumla.

 Mkuu wa Wilaya aliwaeleza wanakijiji na viongozi kuwa walifanya makosa kuuza ardhi yenye ukubwa wa ekari 1000 kinyume cha taratibu, hivyo katika kumdai mwekezaji huyo anayedaiwa kuingia kwenye mashamba na makazi ya wanakijiji wanapaswa kufuata taratibu ili kuweza kupata haki zao kwa utaratibu.

 Ameongeza kuwa mwekezaji ili afanye kazi ni lazima awe na hati miliki  ya eneo na kwamba  Serikali na wananchi kwa ujumla wanahitaji mwekezaji lakini, mwekezaji huyo anapaswa kuwa na faida kwa Serikali na jamii inayomzunguka. Mwekezaji akiwa mzuri  hata wananchi watanufaika.

 Aidha amewataka wanakijiji  kuacha kufanya shughuli kwenye eneo hilo mpaka hapo suluhisho litakapopatikana, wanakijiji wameelezwa kulinda eneo hilo na kuhakikisha hakuna shughuli inayoendelea katika eneo hilo na kwa yeyote atakayekwenda kinyume na taratibu hizo Serikali itachukua hatua.

 “Walinzi wa mali zenu ni ninyi wenyewe, kila mmoja awe mlinzi kuhakikisha kuwa eneo hilo halifanyishiwi shughuli tena mpaka suluhu itakapopatikana , mkibaini mtu anakwenda kinyume na utaratibu huu mtoe taarifa na Kamada wa polisi Wilaya atachukua hatua stahiki” amesema Gondwe.

 Kwa upande mwingine Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe  amesema kuwa mwekezaji ahakikishe anapata hati na kuiwasilisha kwenye ofisi yake kinyume na hapo utaratibu wa kisheria utafuatwa ili kumpokonya ardhi hiyo kwa kupeleka pendekezo la kumyangaya ardhi hiyo kwenye baraza la madiwani kwa sababu atakuwa hana hati.

 Aidha ameongeza kuwa hata akifanikiwa kuipata hati halali Halmashauri haitaweza kumvumilia mtu awe na ekari1000 lazima zitapunguzwe ili ekari nyingine ziweze kufanya shughuli za maendeleo kwenye Halmashauri na Kijiji husika.

Image may contain: 1 person

Mkuu wa Wilaya ya Handeni akizungumza na wanakijiji na mwekezaji.

Image may contain: 3 people, people smiling, people sitting

Mkurugenzi Mtendaji akizungumza na wanakijiji na mwekezaji

Image may contain: 4 people, people sitting and indoor

Baadhi ya wataalamu na wanakijiji

  Image may contain: 1 person, sitting, table and indoor

wanakijiji wakisikiliza kwa makini.

Image may contain: 3 people, people sitting 

Mwenyekiti mstaafu wa Kjiji cha Mkomba akijibu utaratibu alioufuata katika kumuuzia mwekezaji ardhi.








Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa