• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Handeni atembelea kiwanda cha kuchakata mahindi na matunda.

Imerushwa: July 20th, 2018


Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe jana ametembelea eneo la ujenzi wa kiwanda cha kuchakata mahindi na matunda  kinachojengwa katika kijiji cha Michungwani mashariki,Kata ya Segera  kuona maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho.

Mh.Gondwe amewahimiza wawekezaji kuwanufaisha wakulima wa Handeni kwa kununua mazao yanayolimwa katika Wilaya hii kupitia vikundi vya wakulima wadogo wadogo wanaosimamiwa na Wilaya ambao watanufaika na kiwanda moja kwa moja bila kupitia kwa  madalali ambao wakati mwingine watakwamisha wakulima hao kupata haki zao kwa wakati au kutopewa stahiki halali.

Pia alimpongeza mwekezaji huyo kwa kuonyesha jitihada za haraka  baada ya kupewa ardhi ya kiasi cha ekari kumi bure kwani hakuchukua muda akaanza ujenzi wa kiwanda hicho hivyo alimuahidi kupata ushirikiano wowote anaouhitaji na alimuhakikishia upatikanaji wa malighafi  yakutosha kwa kuwa Handeni ina mahindi yakutosha na machungwa yakutosha. Amemueleza mwekezaji huyo kuwa kuna wadau mbalimbali Handeni ambao kwa mwaka huu wameshatoa mbegu mpya ya mazao ya michungwa ya ekari takribani 7000 na kwamba ataendelea kuhamasisha wananchi kupanda hiyo mbegu mpya kwa kushirikiana na maafisa kilimo. 

Mwekezaji wa kiwanda hicho Bw.John Charles Kessy  amesema kuwa ujenzi wa kiwanda hicho kinachojengwa  mpaka kikamilike kitagharimu kiasi cha shilingi bilioni 14 ambapo  ndani yake kutakuwa viwanda vinne(4 in one) yaani  kiwanda cha kuchakata mahindi,kiwanda cha kuchakata matunda,kiwanda cha kuchakata maharage,ulezi na dengu pamoja na utengenezaji wa chakula cha mifugo. Uchakataji utafanyika kwa awamu mbili, awamu ya kwanza wataanza na kuchakata mahindi utakaoanza rasmi mwezi Januari 2019 na kiwanda kitakuwa na uwezo wa kuchakata tani 120 ya mahindi kwa siku.

Amesema kuwa katika kuchakata matunda wakati wanasubiri aina mpya ya machungwa watatumia aina ya machungwa yaliyopo hivyo ameomba wakulima kuhamasishwa kulima mazao ya mahitaji ya kiwanda kwa wingi, Pia ameomba kufanyika kwa mawasiliano ya kuunganisha wakulima na mabenki ili malipo yafanyike moja kwa moja benki badala ya wakulima kupewa fedha mkononi.

Naye Mkurugenzi wa Halmashuri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe amepongeza jitihada za mwekezaji huyo na kwamba pale atakapohitaji ushirikiano wowote ofisi yake iko tayari na amemuahidi kuhamasisha wakulima wa Handeni kulima mazao kwa wingi ili kuhakikisha malighafi ya kiwanda yanakuwepo ya kutosha hatimye kufikia malengo na ndoto ya Mh.raisi ya uchumi wa viwanda katika nchi yetu.

Mh.Diwani wa Kata ya Segera Bw.Yasini Tamimu kwa niaba ya wananchi amesema kuwa wamepata faraja sana kujengwa kwa kiwanda hiki kwani sehemu kubwa ya wananchi wa Handeni ni wakulima wa mahindi na matunda hivyo kupitia kiwanda hiki tutakuwa na soko la uhakika la mazao yetu na bei pia itakuwa nzuri, Ameishukuru sana serikali kwa kuleta mwekezaji Handeni na ameahidi kuwa watampa ushirikiano mwekezaji huyo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa