• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Handeni azindua kampeni elimisha dhidi ya ukeketaji.

Imerushwa: July 22nd, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Toba Nguvila amezindua kampeni ya kupiga vita dhidi ya ukeketaji kwa watoto wakike. Akifungua kampeni hiyo Mh. Nguvila amelishukuru shirika la Kimataifa lisilo la Serikali la Amref Afrika kwa kuchagua Handeni na  kuja kutoa elimu ya kupiga vita dhidi ya ukeketaji kwa watoto wa kike.

Pia amesema jamii ya Handeni bado inaimani potofu ya kukeketa watoto wakike amewakumbusha jamii isijihusishe na vitendo vya kukeketa watoto wa kike kwani kufanya hivyo ni kumnyima haki zake pamoja na kumfanya asijianini mbele ya jamii, hivyo kumuelimsha mtoto wa kike ni kuelimisha jamii nzima.

Kwa kumalizia amewaomba wafanyakazi wote wa Halmashuari ya Handeni kutoa ushirikiano kwa Shirika la Amref ili waweze kutoa elimu dhidi ya kupiga vita suala zima la ukeketaji kwa mtoto wa kike.

Katibu tawala wa Wilaya ya Handeni Mhe. Mashaka Boniphace Mgeta amemshukuru Mh. Rais kwa kumchagua na kumuamini na kumleta Handeni kushiriki kasi ya mageuzi ya maendeleo kwa nchi yetu, amempongeza Rais kwa kujitofautisha na Marais wa Afrika kwa kupunguza gharama za matumizi na kupeleka fedha kwa jamii zifanye kazi za maendeleo. Hivyo amewaomba wafanyakazi na jamii nzima ya Handeni kushirikiana na kufanya kazi kwa umoja kwani Handeni ni ya kwetu sote na maendeleo ni yetu wote.  

Kwaupande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe amemshukuru mkuu wa Wilaya ya Handeni kuzindua kampeni elimisha ya kupiga vita dhidi ya ukeketaji  na kueleza changamoto ya uhaba wa watumishi wa afya kuwa kunauhaba wa asilimia 75% na waliokuwepo wanahudumia  vituo vya afya viwili na zahanati arobaini na nne. Na kunampango wa kujenga vituo vya afya kwa kila tarafa  na zahanati kwenye Halmashauri ya wilaya ya Handeni.

Pia  amewapongeza Amref Afrika kwa kuja kutoa elimu ya mapambano dhidi ya ukeketaji kwenye Hamashairi ya Handeni na kuwahakikishia kuwa watumishi wa Halmashauri ya Handeni wako tayari kuupokea mradi na watatoa ushirikiano mzuri.

Naye afisa mradi elimisha awamu ya tatu Bw. Ibrahim Olekinwaa amemshukuru Mkuu wa wilaya na kumwambia kuwa wameamua kuja kutoa elimu Handeni kwani bado jamii ya Handeni wanaendeleza suala zima la ukeketaji kwa watoto wakike.

 Ameongeza kusema kuwa wanamshukuru Mkurugenzi Mtendaji waHalmashauri ya Handeni kwa ushirikaino wake pamoja na wafanyakazi wote na wamemuomba awaongezee kata tano ambazo wataenda kutoa elimu dhidi ya ukatili wa kijinsia wa kukeketa watoto wa kike.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Toba Nguvila akifafanua jambo kwenye uzinduzi huo.

Katibu tawala Wilaya ya Handeni Mh.Mashaka Boniphace Mgeta, aliyesimama akiongea mbele ya wajumbe wa mradi (hawapo pichani).

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe aliyesimama akitoa ufafanuzi wa changamoto za sekta ya afya kwenye uzinduzi wa mradi huo.

Dr. Serafina Mkuwa kiongozi wa mradi kutoka Amref-Dar es Salaam.

Afisa mradi elimisha Bw.Ibrahim Olekinwaa akieleza madhara yatokanayo na ukeketaji kwa watoto wa kike.

Katibu wa afya Halmashauri ya wilaya ya Handeni Bw. Vendavenda Sumuni aliyesimama.

Wajumbe wa mradi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya kwenye uzinduzi wa mradi elimisha.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI KATIKA NAFASI ZA MWENDESHAJI WA KIFAA CHA BAYOMETRIKI NA AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI February 20, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa