• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Handeni District Council
Handeni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya jamii, Ustawi wa jamii na Vijana
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mazingira na Udhibiti taka ngumu
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Kilimo Umwagiliaji na Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Utamaduni na Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Mfuko wa Jimbo
    • Ratiba ya vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Jarida la Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mwenyekiti CCM Handeni awataka viongozi walioapishwa kufanya kazi kwa weledi

Imerushwa: November 30th, 2019


 Mh. Athumani Malunda aliyasema hayo  katika zoezi la uapishwaji wa viongozi wa serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni ambao ni Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji, viti maalum na wajumbe mchanganyiko  uliofanyika siku tatu kuanzia tarehe 28-30/11/2019 katika Tarafa sita ambazo ni Tarafa ya Mzundu, Mkumburu, Sindeni, Magamba, Mazingara na Kwamsisi

Amesema kiongozi yoyote ambaye hatafuata kanuni taratibu na sharia za uongozi atachukuliwa hatua au kuondolewa katika wadhifa wake hususani migogoro ya ardhi kwamba wasienda kusababisha migogoro ya ardhi lakini waende kusuluhisha tatizo la migogoro ya ardhi katika maeneo yao hasa migogoro kati ya wakulima na wafugaji  na mashamba yaliyouzwa kwa njia  isiyo halali yarudishwe kwa wananchi ili waweze kunufaika na mashamba hayo.

Aidha ametoa onyo kwa viongozi wanaokunywa pombe kupindukia na kusahau jukumu la kutumikia wananchi kuwa watanyang’awa vyeo vyao pindi watakapogundulika, pia amewaasa kuwa mfano kwa wananchi hivyo kuwataka viongozi hao hadi ifikapo Disemba 30 2019 wawe na Bima ya matibabu iliyoboreshwa (ICHF) pamoja na vyoo bora.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe aliwapongeza viongozi wa Serikali za Mitaa kwa kupita bila kupigwa kupitia CCM lakini pia amewaasa  viongozi hao kujitambua nini wanatakiwa kwenda kufanya katika maeneo yao kwaajili ya kuleta maendeleo ya wananchi ikiwepo kuhamasisha kilimo cha mazao mbalimbali hasa mazao yanayostahimili ukame kama mihogo na korosho pamoja na kuhamasisha  wananchi kuchangia shughuli za maendeleo hususani elimu na afya,  pia aliwaasa kuwatanguliza wananchi badala ya wao kujitanguliza.

Makufwe ameongeza kuwa kipindi walichochaguliwa ni kipindi cha kufanya kazi siyo ubabaishaji hasa suala la uaminifu na kujituma ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano. Amesema vijiji havitakiwi kuuza ardhi zaidi ya ekari 50 na wakiuza zaidi ya hapo ni kinyume na taratibu na kwamba watakaofanya hivyo watachukuliwa hatua za sharia

Naye msimamizi wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa Bi. Rachel L. Mbelwa amesema uandikishaji wa wapiga kura ulifanyika kwa amani na utulivu ambapo amesema Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imepata nafasi ya pili Kimkoa na kwa upande wagombea amesema Vjiji vyote 91 na Vitongoji vyote 770 wa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) walipita bila kupingwa  huku Mkoa wa Tanga kitaifa ukishika nafasi ya Tatu kwa wagombea wa CCM kupita bila kupingwa.

 Bi Rachel amesema  viongozi  wa Serikali za Mitaa Handeni Vijijini walioapishwa ni 2,275  wakiwepo Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji, viongozi wa viti maaalum na wajumbe mchanganyiko.

MWISHO.

Taarifa hii imeandaliwa na:

Paulina John

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Handeni DC.

Mwenyekiti CCM Wilaya ya Handeni Mh.Athumani Malunda akizungumza katika zoezi kauapishwaji wa viongozi wa Serikali za Mitaa

Mkurugenzi Mtendaji Handeni DCBw. William Makufwe akitoa neno kwa viongozi walioapishwa

Msimamizi wa uchaguzi Handeni DC Bi.Rachel Mbelwa akielezea jambo katika zoezi hilo

Mwenyekiti wa Halmashauri Handeni DC Mh. Mustafa Beleko akitoa nasaha kwa viongozi wanoapishwa.

Waheshimiwa Kata mbalimbali za Handeni DC wakitoa pongeza kwa viongozi wa CCM waliopita bila kupingwa


Wataalam wa Iadara mbalimbali za Handeni DC wakitoa mafunzo kwa viongozi walioapishwa 

Viongozi wa Serikali za Mitaa Handeni DC waliopita bila kupingwa wakila kiapo



Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HANDENI DC June 04, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • HANDENI DC IMEFANYA KIKAO CHA BARAZA KWA ROBO YA NNE YA MWAKA 2023/2024

    August 12, 2024
  • WANAWAKE HANDENI WAMPONGEZI DKT. SAMIA

    August 09, 2024
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA

    August 06, 2024
  • KUPITIA MAPATO YA NDANI, HANDENI IMETEKELEZEKA MIRADI KEDEKEDE

    October 23, 2023
  • Angalia zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Kwedikwazu Mashariki.
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TASAF
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Tume ya Ajira
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Handeni . Haki zote zimehifadhiwa